Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


 
CHUO cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) kinatarajia kuanza kutoa mafunzo ya kozi ya Uhandisi wa kutengeneza ndege (Air craft maintenance enginearing) kwa ngazi ya cheti na Astashahada ifikapo Novemba, mwaka huu chuoni hapo.

Akizungumza na MTANZANIA jijini Dar es Salaam kwenye maadhimisho ya 13 ya siku ya wahandisi nchini, Ofisa Uhusiano wa NIT, Juma Manday alisema tayari idadi kubwa ya vijana imejitokeza kutaka kusoma kozi hiyo.

“Kwa mara ya kwanza NIT tunatarajia kutoa mafunzo hayo nchini ili watanzania wengi wapate fursa ya kusoma kwani awali iliwalazimu kwenda nje ya nchi ambapo walilipia gharama kubwa,” alisema.

Alisema wanaamini kwamba mafunzo hayo pindi yatakapoanza yatasaidia kuzalisha wataalamu vijana wa kitanzania ambao watakakuja kutengeneza ndege kwa ajili ya nchi yao.
 
“Tunataka kusaidia Taifa letu, vijana hawa wasome hapa hapa badala ya kwenda nje ya nchi ili tuzalishe wataalamu wazalendo ambao wataweza kuja kututengenezea na sisi ndege yetu,” alisema.

Alisema hatua hiyo itasaidia pia kupunguza tatizo la ajira na hatimaye kuinua uchumi wao na Taifa kwa ujumla. 
Source Mtanzania newspaper

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement