ABE, bodi inayotoa kozi mbalimbali kutoka nchini Uingereza,
imeandaa hafla yupi iliyowakutanisha wadau mbalimbali kujadili masuala ya elimu
nchini Tanzania na matokeo yake katika ajira kwa vijana.
Hafla hiyo ilishirikisha watu wenye taaluma mbalimbali kama
ile watoa elimu, wanafunzi, makampuni ya ajira, maofisa rasilimali watu,
wafanyakazi wa makampuni binafsi na serikali, vyombo vya habari na wananchi
wengine wanaoguswa na tatizo hilo.
Katika hafla hiyo, jopo lililoteuliwa na waandaaji
liliongoza majadiliano yaliyowapa changamoto wadau kutafuta njia za kupunguza
tatizo la idadi kubwa ya wanafunzi wanaomaliza masomo kila mwaka ambao wanakosa
nafasi za ajira.
Majadiliano hayo yalitoa hamasa kwa wadau kubainisha ujuzi
na vigezo vinavyohitajika zaidi na waajiri na namna ya kuwasaidia wahitimu
kupata ujuzi huo.
Akizungumza katika hafla hiyo, Mwakilishi wa ABE nchini
Tanzania, Zaituni Ituja alisema “Wote tunafahamu kuwa wahitimu wengi hawana
ajira, lakini pia tunasikia makampuni yanalalamika kuwa hawapati vijana wa
kuwaajiri wenye vigezo. Je tatizo ni makampuni hayajui pa kutafuta wafanyakazi
au wanapata vijana wasiokidhi vigezo? Swali hili ndio chanzo kikubwa cha sisi
kuandaa hafla hii.
Pamoja na majadiliano hayo, wageni walipata muda wa
kufahamiana na kubadilishana mawasialiano ya kibiashara kwa lengo la kujenga
mahusiano kama ilivyokuwadhamira ya hafla hiyo.
ABE inafanya shughuili zake kwa zaidi ya miaka 40 katika
nchi zaidi ya 100 duniani na imewekeza katika kuhakikisha inatoa kiwango cha
elimu cha hali ya juu.
Kozi zinazotolewa ni za masomo ya biashara ambazo zinaweza
kumsaidia mtu kupata shahada ya chuo au kumuwezesha kupanda cheo.
ABE inatoa
kozi za Business Management, Business Start-up na Enterpreneurship, Human
Resouce Management, Marketing Management na Tourism and Hospitality Management.
Kozi hizi zinaweza kusomwa na watu ambao wako kwenye ajira
na wanataka tu kukuza uwezo wao na kupanda cheo au wanaotaka kutumia ABE kama
njia ya kupata nafasi ya kujiunga na vyuo mbalimbali duniani.
ABE wapo
TPHA Building, plot 66 Victoria, Off Ali Hassan Mwingi Road,
Dar es Salaam, TanzaniaMawasiliano
Mobile: +255 713 388 758
Email: zaituni@abeuk.com
Website: www.abeuk.com
Chapisha Maoni