Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo, Azim Dewji akizungumza na baadhi ya wafanyakazi wa MOI na waandishi wa habari (hawapo pichani) mapema leo, (mwenye koti jeupe) ni Mkurugenzi wa Tiba wa taasisi hiyo, Dk. Samwel Swai.

Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

WAUMINI wa dhehebu la Shia nchini wamejitolea kuwezesha matibabu ya watoto 40 waliozaliwa na tatizo la kichwa kikubwa ambao wamelazwa katika Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Mishipa ya Fahamu (MOI).

Akizungumza na waandishi wa habari mapema leo, Mwenyekiti wa jumuiya hiyo, Azim Dewji amesema matibabu hayo yatagharimu kiasi cha Sh. milioni sita.

Mkurugenzi wa Tiba wa MOI, Dk. Swai akiwafafanulia jambo wageni hao.

“Wiki mbili zilizopita tulikuja MOI na tukajitolea uniti 140 za damu lengo ni kufanikisha upasuaji wa watoto hawa na tulikusanya fedha kwa ajili ya kuwezesha matibabu yao.

“Leo tumekuja tena, tumeahidi kuendelea kuchangia damu kupitia shule ya Al-Muntazil. Wananchi wajue kwamba madaktari hawa wanafanya kazi kwa moyo na kwa kujitolea ili kuokoa maisha ya ndugu zetu hawa, ombi langu kwao waje wajitolee damu.

Hapa wakiwa wodini

“Wamenidokeza kila wiki zinahitajika uniti 100 kufanikisha upasuaji, sasa Mungu ametujalia afya nzuri hivyo ni vema nasi tujitolee kusaidia wengine,” ametoa rai.

Amesisitiza “Ukitoa damu hutakufa, jinsi tulivyoumbwa na Mungu ndani ya miezi mitatu hadi minne damu yote uliyotoa inakuwa imerudi, ukitoa damu unapata faida kuu tatu, kwanza unakuwa mtu mwenye huruma, unapata thawabu kwa Mungu na unakuwa umeokoa maisha ya mtu.

Amesema jumuiya hiyo imejiwekea utamaduni wa muda mrefu kuchangia damu katika Mpango wa Taifa wa Damu Salama kila mwaka angalau mara moja lakini sasa wanakusudia kuchangia mara nne hadi tano.

“Tulikuwa tunafanya hivyo kila inapofika mwezi wa Ramadhani sasa tutajitolea si mara moja tu kwa mwaka bali nne hadi tano hivyo nawaalika na waumini wa wananchi wengine tuungane kuchangia damu,” amesema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement