Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

KC2Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) Profesa. Mohamed Janabi akielezea jambo wakati wa ziara ya Wajumbe wa Kamati ya Huduma za Jamii wa Bunge la Uganda waliotembelea Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam. Wabunge hao wametembelea Taasisi hiyo ili kujionea namna inavyofanya majukumu yake

 NA VERONICA ROMWALD – DAR – ES SALAAM

Kamisheni  ya Tume ya Utumishi wa Bunge la Uganda kuvutiwa na mafanikio ya utoaji huduma za kutibu magonjwa ya moyo zinazotolewa katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI).

Kamisheni hiyo jana ilifanya ziara ya kujifunza katika Taasisi hiyo mapema asubuhi ikiongozwa na Kamishna wake, Ceclia Barbara.

Akizungumza na waandishi wa habari, Kamishina huyo alisema JKCI imepiga hatua kubwa na kutoa huduma bora kwa watanzania hali ambayo imesaidia kupunguza idadi ya rufaa za wagonjwa wa moyo kwenda nje.

KC4Baadhi ya Wabunge kutoka Uganda wakifuatilia Maelezo kuhusu namna JKCI inavyofanya kazi wakati wa ziara yao katika Taasisi hiyo leo Jijini Dar es Salaam.

“Uganda tunatoa huduma za tiba ya moyo ingawa tuna changamoto nyingi zinaikabili sekta ya afya, lakini wenzetu wameyapata kwa muda mfupi wa takriban miaka mitatu wamesaidia watanzania wengi,” alisema.

Alisema kutokana na hali hiyo ndiyo maana waliona vema kufanya ziara hiyo ya kujifunza.

“Sisi kama wanasiasa tumejifunza vitu vingi hapa kwa mfano tumeona uwekezaji mkubwa uliofanywa na serikali hapa, na kuanzia sasa mnaweza kuona wataalamu wetu wengi wakija kujifunza,” alisema.
 KC5
Baadhi ya Wabunge kutoka Uganda wakiwa katika sehemu ya mapokezi ya kuingia Wodi ya Watoto.

Aliongeza “Lakini pia tumetoa ombi letu kwa uongozi wa JKCI ili tushirikiane nao watusaidie wataalamu wake waje nchini mwetu ili kutoa mafunzo haya.

alisema ipo haja kwa nchi zilizopo kwenye jumuiya ya Afrika Mashariki kushirikiana kwa dhati na kujifunza miongoni mwao ili kusaidia wananchi wengi zaidi.
 KC1
Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Profesa. Mohamed Janabi akipeana mkono na Kiongozi wa Msafara wa baadhi ya Wabunge kutoka Uganda Mhe. Cecilia Barbara wakati wa ziara yao katika Taasisi hiyo kwa lengo la kujifunza.

“Niliwahi kufika Tanzania mara kadhaa, na kila ninapokuja naona mabadiliko makubwa hasa katika sekta ya afya, naipongeza serikali ya Tanzania kwa uwekezaji uliofanyika  katika sekta ya afya… kuja kwetu hapa leo (jana) tumehamasika mno,” alisema.

Mkurugenzi wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi akizungumza alisema wamepokea ombi la Kamisheni hiyo kwamba wapo tayari kuwapa mafunzo.

“Tutakwenda kuwapa mawazo ili nao wapige hatua,  takwimu zinaonesha Uganda kwa miaka mitano wamehudumia wagonjwa 850 JKCI imeweza kuhudumia wagonjwa 1000 kwa kipindi cha mwaka 2016/17.
 KC3
Mwenyekiti wa Kudumu wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Mussa Zungu akizungumza jambo mbele ya Wabunge kutoka Uganda walipotembelea JKCI. Kutoka kushoto ni Kiongozi wa Msafara wa Wabunge kutoka Uganda Mhe. Cecilia Barbara na Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI Profesa. Mohamed Janabi (katikati).

“Kipindi cha mwaka 2014 tuliona wagonjwa 5000 lakini mwaka huu hadi sasa tumeona wagonjwa 40,000, tayari tumewafanyia upasuaji wa bila kufungua kifua kutibu magonjwa ya moyo wagonjwa 620 na wagonjwa 150 tumewatibu kwa njia ya kufungua kifua,” alisema.

Aliongeza “Leo (jana) tumefanya upasuaji mkubwa wa kuweka benti kubwa kwenye moyo iitwayo kitaalamu CRTD na tunatarajia kuwafanyia wagonjwa 20 upasuaji huo ambao ikiwa wangeenda India ingegharimu Sh milioni 120 kwa kila mgonjwa mmoja lakini hapa JKCI wanagharimu Sh milioni 35 hadi 40 pekee.

Alisema changamoto inayowakabili sasa ni ufinyu wa nafasi ambapo wana jumla ya vitanda 128 kwa ajili ya watoto na watu wazima.

“Lakini hili linafanyiwa kazi na serikali, iwapo tutapata nafasi kubwa nchi itapiga hatua zaidi,” alisema.

Akizungumza kwa niaba ya Spika wa Bunge la Tanzania, Mwenyekiti wa Bunge, Mussa Hassan Zungu alisema kwa kuwa wajumbe wa kamisheni hiyo wamekuja kutizama masuala ya afya nchini walipendekeza kuwafikisha kujifunza JKCI.
 KC6
Mkurugenzi Mtendaji wa  JKCI)Profesa. Mohamed Janabi (mwenye tai nyekundu) akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya Wabunge kutoka Uganda walipotembelea Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) kwa lengo la kujifunza leo Jijini Dar es Salaam

“wamefurahi mno na wameona jinsi ambavyo Tanzania tumeweza kupunguza idadi ya wagonjwa tunaowapa rufaa kwenda India kutoka 300 hadi wanne mwaka jana, ni kutokana na uwekezaji huu tuliofanywa,” alisema.

Alisema ili kuongeza ufanisi wa huduma zinazotolewa katika taasisi hiyo serikali imepatia fedha zote za maendeleo (OC) ambazo waliziomba.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement