Wananchi wakimsikiliza kwa umakini Nyamkinda.
Diwani wa Msigani Israel Mushi (mwenye tisheti nyekundu na koti la khaki) akiangalia moja ya ramani zilizopimwa katika hatua ya awali.
Diwani Israel akifurahia jambo na wananchi wake.
Diwani huyo amesema upimaji huo utasaidia serikali kupata mapato yake stahiki pindi utakapokamilika na kwamba utasaidia kupunguza na hatimaye kumaliza kabisa migogoro ya ardhi ndani ya kata hiyo.
Mkurugenzi wa Mipango Miji na Vijiji wa Wizara ya Ardhi,
Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Profesa John Lupala amesema wizara inatambua upimaji huo na kwamba inafuatilia kwa ukaribu.
"Utasaidia mno katika kufikia lengo letu tulilojiwekea la kutambua maeneo yasiyo rasmi na kuwarasisha wananchi, tumelenga kumilikisha hati 400,000 katika mwaka huu wa fedha," amesema.
Wananchi wakifuatilia kwa makini ufunguzi huo.
Wananchi wakifuatilia jambo kwa umakini wakati wa ufunguzi huo.
Picha zote na Veronica Romwald.
Chapisha Maoni