Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


http://www.channelten.co.tz/wp-content/uploads/2017/08/maxresdefault-1024x576.jpgPicha na mtandao

Na Veronica Romwald – Dar es Salaam

MSIMAMO wa serikali ya awamu ya tano wa kupiga marufuku wasichana wanaobeba ujauzito wakiwa shule ya msingi na sekondari kurejea shuleni baada ya kujifungua.

Rais John Magufuli alitangaza marufuku hiyo hivi karibuni akiwa Chalinze mkoani Pwani.

Alinukuliwa “katika utawala wake wasichana watakaobeba mimba wakiwa shuleni hawataruhusiwa kurudi katika mfumo rasmi hata baada ya kujifungua.

“Labda waende kwenye mfumo usio rasmi kwa mfano huko kwenye vyuo vya ufundi stadi ikiwamo VETA na kwingineko,” alinukuliwa akisema.

Alisisitiza mwanamume ambaye atapatikana na hatia ya kumpachika mimba mtoto wa shule, atafungwa jela miaka 30 na kutumia nguvu alizotumia kumpachika mimba msichana huyo, kufanya kilimo akiwa gerezani.

"Mashirika haya yasiyo ya serikali yanastahili kuenda kufungua shule kwa wazazi, lakini hayastahili kuilazimisha serikali kuwarejesha shuleni. Ninatoa elimu ya bure kwa wanafunzi ambao wameamua kusoma, na sasa mnataka niwaelimishe wazazi,"  alihoji.

Msimamo huo wa serikali ulipokelewa kwa mitizamo miwili tofauti kwenye jamii, wapo ambao wanaunga mkono suala hilo na wapo ambao wanapinga hasa mashirika yasiyo ya kiserikali.
 http://www.mwananchi.co.tz/image/view/-/3272568/highRes/1346185/-/maxw/600/-/ae7ucpz/-/Mimba.jpg
Wasemavyo wazazi

Maimuna Ally mkazi wa Mbezi Luis jijini Dar es Salaam anasema anaunga mkono msimamo huo uliotolewa na serikali kwamba wasichana walijiachia mno na kuendekeza mapenzi badala ya masomo.

“Wengi waliona hakuna umuhimu wa masomo, binafsi nimeshaongea mno na wanangu lakini hawasikii na wala walikuwa hawataki kubadilika, kwa amri hiyo ya Rais Magufuli naamini watabadilika na kurejea kwenye mstari,” anasema.

Wakati Maimuna akikubaliana na msimamo huo, Juma Karim mkazi wa Sinza Kijiweni anaupinga huku akisema kwamba una mkandamiza mtoto wa kike.

“Unajua si wote wanaobeba ujauzito wanakuwa wamependa, kuna ambao wanabakwa au wanashawishiwa na wanaume ‘wakware’ mwisho wa siku kwa kuwa jamii nayo ipo kimya na haipendi kueleza watoto ukweli wanajikuta wamepata ujauzito,” anasema.

Anaongeza “Nakubali wapo ambao wanajihusisha na mahusiano ya kimapenzi wakiwa shuleni kwa kupenda wenyewe, lakini naona wengi huwa ni kwa kushawishiwa na wengine kwa kubakwa.

Anasema kutokana na hali hiyo serikali ilipaswa kuangalia upya msimamo wake. Hata hivyo bado serikali imesisitiza juu ya msimamo wake huo.

Hawa ni wazazi hao ambao wanawakilisha mawazo ya wazazi walio wengi katika jamii, lakini pamoja na yote hayo lazima kila mmoja wetu ajiulize swali la msingi kwamba je, hatima ya mtoto wa kike ipo mikononi mwa nani.

Wahenga na malezi

Upo msemo wa wahenga usemao, kuzaa si kazi, kazi kule mwana. Kwamba ni rahisi kulea mtoto akiwa tumboni mwa mama lakini ni kazi kumlea akiwa tayari amezaliwa.

Mzee Mussa Faustine (78) Mkazi wa Manzese, jijini hapa anasema kwa kawaida mtoto akiwa tumboni hitaji lake kuwa huwa ni chakula cha kutosha kutoka kwa mama yake ili aumbike vema.

“Mtoto akizaliwa katika mwaka sifuri hadi miaka 18 mbali na chakula bora mahitaji yake huongezeka, huhitaji kupata haki zake za msingi kuanzia kula, malazi, elimu, afya bora, ulinzi wa kutosha na malezi bora kutoka kwa wazazi na jamii nzima iliyomzunguka,” anasema.

Changamoto

Hata hivyo, ingawa inasisitizwa kwamba watoto wote wana haki sawa bado kuna changamoto nyingi zinazomkabili mtoto wa kiume.

Kwa muda mrefu kumekuwapo mila na desturi ambazo zinamkandamiza mtoto wa kike hali ambayo imekuwa ikimfanya akose haki zake nyingi za msingi hasa ya kusoma.

Mtoto wa kiume anapozaliwa kwenye jamii anaonekana bora zaidi kuliko wa kike.

Kwa mfano yapo baadhi ya makabila ambayo yanaona mtoto wa kike hastahili kabisa kwenda shule badala yake yeye ni wa kusubiri kuolewa kwenda kuitunza familia yake.


Ofisa wa Mradi wa Shirika lisilo la Kiserikali la African Youth and Adolesence Network on Population and Development (Afriyan), Jennifer Kayombo akizungumza na mwandishi wa makala haya hivi karibuni
 
Mtizamo wa kijana

Ofisa wa Mradi  huyo anasema bado jamii inahitaji kupatiwa elimu ya kutosha ili kuondokana na mila na desturi zinazoendelea kumkandamiza mtoto wa kike.

“Serikali imetangaza msimamo wake, lakini binafsi naona nguvu kubwa sasa inapaswa kuwekezwa kwenye kupeleka elimu kwa jamii kuachana na mila na desturi zinazomkandamiza mtoto wa kike,” anasema.

Anasema mtoto wa kike anastahili kupata haki ya elimu kama ilivyo kwa mtoto wa kiume na kwamba ili kumkomboa kutokana na changamoto ya ndoa na mimba za utotoni anapaswa kuopatiwa elimu sahihi ya afya ya uzazi.

“Elimu hiyo itolewe kwa vijana wote bila kuwabagua, vijana wakijitambua naamini kabisa ndoa na mimba za utotoni zitapungua kama si kuisha kabisa na hivyo wasichana watapata nafasi ya kusoma na kumaliza masomo yao wakiwa kwenye mfumo rasmi,” anasema.

Anaongeza “Vijana lazima wapatiwe elimu ya afya ya uzazi, wajitambue, ni muhimu mno kwani kundi hili takwimu zinaonesha ni zaidi ya asilimia 60 ya watanzania wote waliopo nchini, na elimu pekee ndiyo ambayo itawakomboa.

“Tumegundua jamii bado inaishi kwa kuamini mila na desturi ambazo kimsingi zinamkandamiza kijana hasa msichana. Familia nyingi hazimpi msichana fursa ya kutoa maamuzi (hana sauti kwenye familia),” anasema.

Mfano wa Singida

Ofisa Mradi huyo wa Afriyan anasema shirika hilo limewahi kwenda kutembelea kijiji kimoja huko mkoani Singida ambapo walikutana na dada mwenye umri wa miaka 17 ambaye alikuwa tayari amezalishwa watoto wawili.

“Dada huyo alilazimika kuacha shule kutokana na kubeba ujauzito, tulimuuliza maswali mbalimbali jambo lililotusikitisha alitueleza hakupata elimu kabla juu ya madhara yatokanayo na kujamiiana.

“Dada huyo alitueleza kwamba alianza kujamiiana akiwa darasa la tatu, alitueleza hakuwa amepata kujifunza elimu ya afya ya uzazi hapo kwanza, hivyo hakuwa anajua kuna kupata mimba, alijikuta tayari ni mjamzito na hakuweza tena kuendelea na shule hadi leo yupo nyumbani akilea watoto wake hao,” anasema.
 https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEj0UPUX8ta4GFRdYXzWOzZVZARjudbdWUm0k0O2zztFqR6o4cvew1xLrTvOG3aVbT44SakkNpk6LEZ92XpdlZLKN4zn3PWilC1GClt1rWdWYA7B4oQ4AX-JbuWoGqzJTuJuPYoAdvJiAaDm/s1600/PICHA+3.JPG
Kauli ya Waziri

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu (pichani) anasema Wizara imejipanga kuendelea kuelimisha wazazi kuzingatia malezi ya watoto wao.

“Rais Magufuli ametoa msimamo wa serikali, mimi amenipa dhamana ya kusimamia sera ya maendeleo ya mtoto na ninamsaidia kusimamia katika masuala ya afya, maendeleo ya jamii, jinsia, wazee na watoto.

“Si kwamba wasichana wanaopata ujauzito hawatasoma, watasoma lakini si kwenye mfumo rasmi bali mfumo usio rasmi labda Veta na ufugaji,” anasema.

Anaongeza “Hivyo kwa sababu tuna dhamana hii ya  kusimamia maendeleo ya watoto wakike na wakiume nguvu kubwa sasa ni kuendelea kuwahimiza na kuwashawishi wazazi kutimiza wajibu wao kikamilifu katika malezi ya watoto.

“Wazazi wengi wapo ‘bize’ kutafuta fedha… kwa hiyo Idara yake ya Maendeleo ya Jamii, tutaendelea kuwahimiza wakumbuke wajibu wao, aidha tutaendelea kuwahamasisha vijana (wasichana) kuzingatia masomo,” anasema.

Kampeni maalumu

“Tunataka mtoto wa kike azingatie elimu badala ya mambo mengine, rai yangu kwa mashirika yasiyo ya serikali, twendeni kwenye kila kijiji na kila mtaa tumwambie mtoto wa kike, tunataka kila mmoja aseme sishabii mapenzi, elimu ndiyo mpango mzima,” anasema.

Anaongeza “Tutawajengea uwezo watoto wa kike, tutaimarisha elimu ya afya ya uzazi katika shule za msingi na sekondari.

Anasema lengo ni kupunguza idadi ya wasichana ambao wanapata ujauzito wakiwa katika umri mdogo kabla ya miaka 18.

“Takwimu zinaonesha katika kila wasichana 100, wenye umri wa chini ya miaka 18 nchini wasicaha 27 wanapata ujauzito, tunataka kumfikia kila msichana katika kila mtaa na kila kijiji ajitambue ili aweze kuzingatia masomo badala ya mambo mengine,” anasema.

Anaongeza “Endapo mtoto anabakwa kazi yetu (Wizara) ni kuhakikisha wabakaji wanafikishwa kwenye vyombo vya dola, ni vema jamii, wazazi na walezi watoe ushirikiano tafiti zinaonesha watoto wanabakwa na watu wa karibu yetu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement