Katuni na mtandao
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
NDOA na mimba za utotoni bado zinatajwa kuwa kikwazo
kikubwa kwa mtoto wa kike kuweza kufikia ndoto zake za baadae nchini kama
ilivyo kwa mtoto wa kiume.
Pamoja na jitihada zinazofanywa na serikali kwa
kushirikiana na wadau mbalimbali wa maendeleo takwimu zinaonesha tatizo hilo
linazidi kuongezeka.
Hali hiyo inatajwa kuchangiwa zaidi na mila potofu na
desturi za baadhi ya makabila ambazo kwa namna moja au nyingine zinakandamiza
haki za mtoto wa kike.
Kwa mfano yapo baadhi ya makabila ambayo hadi leo yanamuona
mtoto wa kike ni sawa na bidhaa inayofaa kuuzwa na kununuliwa hasa pindi tu
anapovunja ungo.
Wakati mtoto wa kike akionekana kuwa sawa na bidhaa mambo
ni tofauti kwa mtoto wa kiume ambaye huendelea kupatiwa mahitaji na haki zote
za msingi hususan elimu.
Watoto wa kike mara nyingi tunashuhudia katika baadhi ya
maeneo wakikatishwa masomo yao na kuozeshwa.
Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linaloshughulikia
Idadi ya Watu Duniani (UNFPA) ya mwaka 2016, inaeleza wasichana wana fursa
ndogo ya kumaliza shule ikilinganishwa na wavulana.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa Oktoba 20, mwaka jana huko Visiwani Zanzibar, inaeleza wasichana wako katika hatari zaidi ya kukabiliwa na ndoa za utotoni, ajira za watoto, ukeketaji na matendo mengine ya udhalilishaji.
Ripoti hiyo iliyozinduliwa Oktoba 20, mwaka jana huko Visiwani Zanzibar, inaeleza wasichana wako katika hatari zaidi ya kukabiliwa na ndoa za utotoni, ajira za watoto, ukeketaji na matendo mengine ya udhalilishaji.
Inataja asilimia 42 ya wasichana Barani Afrika, huolewa
wakiwa na umri wa chini ya miaka 18 na kwamba kwa wastani watoto wa kike wawili
kati ya watano huolewa kabla ya kufikisha umri huo wa miaka 18 nchini.
Kulingana na ripoti hiyo ndoa za utotoni, ajira za watoto,
ukeketaji,
na matendo mengine ya udhalilishaji yanayodhoofisha haki na afya ya msichana yanatishia matumaini ya ajenda ya kimaendeleo ya dunia.
na matendo mengine ya udhalilishaji yanayodhoofisha haki na afya ya msichana yanatishia matumaini ya ajenda ya kimaendeleo ya dunia.
Kwamba, matendo hayo yanaathiri wasichana na kuvunja haki
zao za kibinadamu kuanzia wakiwa na umri wa miaka 10 na kufanya washindwe
kutimiza ndoto zao katika maisha yao hapo baadae.
Mwakilishi wa UNFPA- Tanzania, Dk. Hashina Begum
Ripoti hiyo inasisitiza zaidi ya nusu ya wasichana 60
milioni walio na umri wa miaka 10 wanaishi katika nchi 48 zenye ukosefu mkubwa
wa usawa wa kijinsia.
Kwa mujibu wa ripoti hiyo, inaonesha kati ya vijana milioni
125 walio na umri wa miaka 10 hii leo, kati yao wasichana ni milioni 60.
Ripoti
ya WHO
Katika utafiti uliofanywa na Shirika la Afya Duniani (WHO)
na matokeo kuchapishwa Januari, 2016 Tanzania ilitajwa kuwa ni nchi ya tatu
barani Afrika miongoni mwa nchi zenye viwango vya juu vya matukio ya ndoa za
utotoni.
Ripoti hiyo inaeleza matukio ya ndoa na mimba za utotoni nchini yapo kwa kiwango cha asilimia 28.
Ripoti hiyo inaeleza matukio ya ndoa na mimba za utotoni nchini yapo kwa kiwango cha asilimia 28.
Ripoti
ya NBS
Matokeo ya utafiti wa Idadi ya watu na Afya Tanzania (TDHS,
2010) uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini (NBS) nayo yanaonesha asilimia 37 ya watoto wa kike Tanzania huolewa kabla ya kufikisha miaka 18.
kwa mujibu wa utafiti huo, Mkoa wa Shinyanga unaoongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha ndoa za utotoni kwa kiwango cha asilimia 59 ukifuatiwa na Mkoa wa Tabora wenye asilimia 58, Mara asilimia 55, Dodoma asilimia 51, Lindi asilimia 48, Mbeya asilimia 45, Morogoro asilimia 42, Singida asilimia 42, Rukwa asilimia 40 na Ruvuma wenye asilimia 39.
Ripoti hiyo inataja mikoa mingine yenye idadi kubwa ya ndoa za utotoni ni Mwanza asilimia 37, Kagera asilimia 36, Mtwara asilimia 35, Manyara asilimia 34, Pwani asilimia 33, Tanga asilimia 29, Arusha asilimia 27, Kilimanjaro asilimia 27, Kigoma asilimia 29, Dar es Salaam asilimia 19 na Iringa ambao una asilimia nane.
2010) uliofanywa na Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini (NBS) nayo yanaonesha asilimia 37 ya watoto wa kike Tanzania huolewa kabla ya kufikisha miaka 18.
kwa mujibu wa utafiti huo, Mkoa wa Shinyanga unaoongoza kwa kuwa na kiwango kikubwa cha ndoa za utotoni kwa kiwango cha asilimia 59 ukifuatiwa na Mkoa wa Tabora wenye asilimia 58, Mara asilimia 55, Dodoma asilimia 51, Lindi asilimia 48, Mbeya asilimia 45, Morogoro asilimia 42, Singida asilimia 42, Rukwa asilimia 40 na Ruvuma wenye asilimia 39.
Ripoti hiyo inataja mikoa mingine yenye idadi kubwa ya ndoa za utotoni ni Mwanza asilimia 37, Kagera asilimia 36, Mtwara asilimia 35, Manyara asilimia 34, Pwani asilimia 33, Tanga asilimia 29, Arusha asilimia 27, Kilimanjaro asilimia 27, Kigoma asilimia 29, Dar es Salaam asilimia 19 na Iringa ambao una asilimia nane.
Meneja wa Afya ya Uzazi na Ujinsia na Afya ya Mama na Mtoto wa UNFPA-Tanzania,
Felister Bwana anasema hali hiyo inachangiwa zaidi na ukosefu wa elimu sahihi
ya afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana.
Anasema jamii nyingi hasa zilizopo Barani Afrika zinachukulia
suala la afya ya uzazi na ujinsia, mahusiano na kujamiiana kwa ujumla ni
masuala ambayo hayapaswi kuzungumzwa.
“Wanaamini ni mwiko kuzungumzia masuala hayo na kamwe
huwezi kukuta wazazi wakizungumza na watoto wao kuwaeleza ukweli juu ya mambo
hayo au baba anaona ni jukumu la mama kuwaeleza watoto wake hali hiyo inafanya
vijana kutafuta taarifa wenyewe shida inatokea pale wanapopewa taarifa ambazo
si sahihi,” anasema.
Mkakati
wa kuwakomboa
Felister anasema kutokana na hali hiyo, UNFPA, Kanda ya
Afrika iliamua kuanzisha mradi wa Amua Accelerator kwa lengo la kutafuta mbinu
bunifu kukabiliana na tatizo la ndoa na mimba za utotoni nchini.
Anasema ili kufanikisha mradi huo UNFPA imeshirikiana kwa
ukaribu na serikali pamoja na mashirika likiwamo Shirika lisilo la Kiserikali
la Sahara Sparks na Mulika Tanzania.
“Mradi huu
unatekelezwa katika nchi nne ikiwamo Tanzania, Kenya, Rwanda na Uganda,
tunawakusanya vijana na wao wanatakiwa kubuni njia (mbinu) ambazo zitatumika
kufikisha ujumbe sahihi wa afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana wenzao,”
anasema.
Anasema pamoja na kwamba lengo ni kufikisha ujumbe sahihi
lakini lengo jingine ni kuwatengeneza fursa ya ajira vijana kupitia ubunifu
wao.
“Tuliona kwa kuwa tatizo la ndoa na mimba za utotoni
linawakabili vijana, tuliamini kwamba wanafahamu tatizo lipo wapi ingawa
tunafahamu kwamba vijana wengi bado
hawana elimu sahihi kuhusu afya ya uzazi na ujinsia.
“Lakini pia hawajafikiwa na huduma za afya ya uzazi na
ujinsia, tumebaini pia hata wale waliofikiwa na huduma tumebaini watoa huduma
wengi si rafiki kwa vijana wanaokwenda kufuata huduma hizo hii imesababisha
wengi kuwa waoga na kushindwa kujiamini kufika kwenye vituo vya kutolea huduma
hizi.
“Vile vile vijana
wengi waishio maeneo ya vijijini pia hawapati taarifa sahihi kuliko hawa
waishio mjini. Kuna suala la mila na desturi pia ambapo katika jamii nyingi
inaonekana ni mwiko kutamka masuala ya afya ya uzazi na ujinsia.
“Yaani masuala ya mahusiano na kujamiiana kwa ujumla huwezi
kukuta mzazi anamueleza kijana wake au baba anaona ni jukumu la mama kuwaeleza
watoto wake hali hiyo inafanya vijana kutafuta taarifa wenyewe shida inatokea
pale wanapopewa taarifa ambazo si sahihi,” anasema.
Anaongeza “Hivyo, kupitia mradi huu wa Amua Acceleration
tuliona wakati umefika sasa kuwaita vijana wenyewe na kuwashirikisha ili wabuni
mbinu zitakazosaidia kuwafikishia ujumbe sahihi vijana wenzao.
Anasema kwa kiwango kikubwa vijana waliofanikiwa kufikia
mwisho wa mchakato huo wamefanikiwa kubuni mbinu za kisasa ambazo anaamini zitatumika
kufikisha ujumbe sahihi wa afya ya uzazi na ujinsia kwa vijana wenzao na hivyo
kupunguza ukubwa wa tatizo hilo.
Mchakato
ulivyokuwa
Meneja Mradi wa Sahara Sparks, Adam Mbyallu (pichani) anasema
waliwakutanisha wadau wa sekta ya afya na vijana wenyewe ambao walijadiliana na
kuainisha changamoto zinazowakabili vijana kuhusu suala zima la afya ya uzazi
na ujinsia.
“Wadau hao waliainisha matatizo manne ambayo ni ambayo ndoa
za utotoni, mimba za utotoni, afya ya hedhi, maambukizi ya virusi vya ukimwi na
ukimwi. Wadau walikubalina suala la ndoa za utotoni liwe ajenda kuu la mradi,”
anasema.
Anasema tulienda mbali zaidi na kuwauliza wadau iwapo wanadhani
tatizo hilo linachangiwa na nini hasa na wakatueleza ni kutokana na ukosefu wa
elimu sahihi ya afya ya uzazi na ujinsia.
“Vijana walisisitiza kwamba hakuna upatikanaji wa huduma
rafiki za afya ya uzazi na ujinsia, vituo vingi vimewekwa kwenye kliniki za
uzazi na watoa huduma si rafiki,” anasema.
Anasema wadau hao walieleza pia jambo jingine linalochangia
ongezeko la ndoa na mimba za utotoni ni ushiriki mdogo wa wanamume katika
kutatua changamoto za uzazi salama na ujinsia.
“Wanaume wengi wanadhani kuongea na binti kuhusu masuala
hayo ni jukumu la mama, shangazi au bibi yake,” anafafanua.
Anasema wadau walisema kuna mkanganyiko wa sheria ya ndoa
ya 1971 ambayo inaruhusu mtoto kuolewa akiwa na umri wa miaka 14/15 kwa ruhusa
ya wazazi wake.
“Wakati sheria ikiruhusu hivyo, wataalamu wa afya wanasema
ni vema msichana kujifungua akiwa na umri wa miaka juu ya 18 kwamba anakuwa
viungo vyake vimekomaa,” anasema.
Anasema kutokana na uwepo wa ndoa na mimba za utotoni
zimechangia ongezeko la idadi ya vifo vitokanavyo na uzazi.
“Kwa hiyo tulipokea mawazo 373 ambayo yalitoka kwa vijana
wenyewe na baada ya kuyachambua tulipata vikundi sita ambavyo vine kati yake vimeibuka
na ushindi na kujinyakulia Dola 6,000 sawa na Sh. Milioni 14 kila kimoja,”
anasema.
Kauli
za washindi
Mwakilishi wa kikundi cha Harakati za lucy Gwamaka Mwabuka
anasema wametengeneza katuni ambayo wataitumia kufikisha ujumbe wao kupitia
mtandao wa youtube.
“Tumekusudia pia baadae kuingia mkataba na chaneli
mbalimbali nchini ambazo zitarusha katuni hizi zitakazotengenezwa katika
‘episods’ tofauti tofauti, Lucy anawakilisha wasichana wengi,” anasema.
E-Shangazi
Mwakilishi wa kikundi hiki, Debora Peter anasema E-
Shangazi ni shangazi wa mtandao ambaye atakuwa akitoa elimu ya afya ya uzazi na
ujinsia kwa njia ya facebook.
“Katika jamii nyingi za ki-Afrika shangazi ni mtu muhimu
ambaye vijana humshirikisha mambo mengi, kwa hiyo kupitia shangazi huyu wa
mtandao Kijana, mzazi au mlezi ataweza kumuuliza swali lolote shangazi huyu
naye atampa majibu sahihi kupitia akaunti ya ‘facebook messenger’,” anasema.
Mkwawa
Art Space
Kundi hili ambalo makazi yake yapo kule mkoani Iringa
lenyewe limejipanga kutumia sanaa kufikisha ujumbe kwa vijana, wazazi na
walezi.
Maisha
package
Mwakilishi wa kundi hili, anasema wao wamebuni ambapo ndani
yake watakuwa wakiuza taulo za kike, kondomu za kiume na kwamba wataweka
kipeperushi chenye taarifa sahihi kuhusu afya ya uzazi na ujinsia.
“Kwa kuzingatia umri, tumetengeneza vitita viwili, kuna
ambacho hakitakuwa na kondomu za kiume ndani yake (Maisha package plain) ambazo
mzazi anaweza kumnunulia mtoto wake pia na akapata kipeperushi chenye taarifa
sahihi kuhusu afya ya uzazi na ujinsia,” anasema.
Mwakilishi
wa UN
Akizungumza katika hafla ya kukabidhi zawadi kwa
washindi hao, Mwakilishi Mkazi
wa Mashirika ya Umoja wa Mataifa nchini (UN -TANZANIA), Alvaro Rodriguez anasema
kupitia mradi huo ambao una malengo sawa na Malengo ya Maendeleo Endelevu
(SDGs), UN wataendelea kushirikiana na Serikali ya Tanzania katika kuboresha
huduma za afya kwa kutoa elimu ya afya ya uzazi vijana.
“Mradi huu ni sehemu
ya mpango wetu wa kuhakikisha vijana wanafikia malengo yao, nawashukuru UNFPA
kwa kuendesha mradi huu kwa ajili ya vijana Tanzania,” anasema Rodriguez
Anaongeza “Katika
kipindi hiki ambacho Tanzania inaelekea uchumi wa kati kunahitajika kuwa na sera
na mipango ambayo itaiwezesha nchi kuwa na uwiano wa umri na kutasaidia kuwepo
kwa nguvu kazi na hasa vijana ambayo itafanya kazi na kusaidia uchumi kukua.
Makala haya kwa mara ya kwanza yametoka leo kwenye gazeti la MTANZANIA
Makala haya kwa mara ya kwanza yametoka leo kwenye gazeti la MTANZANIA
Chapisha Maoni