Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
http://blog.ikulu.go.tz/wp-content/uploads/2015/11/3.jpgRais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Joseph Magufuli akimjulia hali mmoja wa wagonjwa waliolazwa kwenye wodi ya Taasisi ya Mifupa Muhimbili(MOI)

MIAKA MIWILI YA MH. DKT. JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI  - SEKTA YA AFYA YAPATA MAFANIKIO MAKUBWA. TUNAKUPONGEZA KWA KUWEKEZA KWENYE AFYA NA USTAWI ZA WATANZANIA

Katika kipindi cha miaka miwili ya uongozi wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania , Dkt. John Pombe Magufuli,Serikali kupiti Wizara ya Afya imeleta maboresho makubwa ili kuhakikisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi. Tunajivunia mambo makuu 6.

HALI YA UPATIKANAJI WA DAWA YAZIDI KUIMARIKA

       Hali ya upatikanaji wa dawa inaendelea kuimeimarika ambapo hadi Oktoba 2017, asilimia 80 ya dawa muhimu (Essential Medicine)135 zinazohitajika katika vituo  vya kutolea huduma za afya vya Serikali nchini zinapatikana kwenye maghala ya Bohari ya Dawa (MSD) ikilinganishwa na  36%  iliyokuwepo mwezi Juni 2015. Hili imefanikiwa kutokana na uamuzi wa Mhe Rais Dr John Magufuli wa kuongeza fedha kwa ajili ya ununuzi na usambazaji wa Dawa, Vifaa, na Vifaa Tiba, pamoja na Chanjo kutoka shilingi Bilioni 31 mwaka 2015/2016 mpaka  Shilingi Bilioni 251.5 mwaka 2016/2017 na kufikia shilingi Bilioni 269 kwa mwaka 2017/2018.

Bei ya dawa muhimu zaidi imepungua kwa wastani wa asilimia 30 kutokana na uamuzi wa Serikali kununua dawa moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji. Mfano dawa  ya kupambana na maambukizi ya backteria (amoxicillin/Clavulanic Acid Potassium 625mg) yenye vidonge 15 awali ilikuwa inauzwa na MSD kwa shilingi 9,800/=, kuanzia Julai 2017 inauzwa shilingi 4,000/=.

HUDUMA ZA MATIBABU YA KIBINGWA ZAIMARIKA NA HIVYO KUPUNGUA KWA WAGONJWA WANAOPELEKWA NJE YA NCHI KWA AJILI YA MATIBABU

·       Huduma za Matibabu ya kibingwa zimeimarishwa na hivyo kuwezesha huduma hizi kupatikana kwa wananchi wengi na kwa gharama nafuu.  Hatua hii pia imewezesha kupungua kwa Idadi ya wagonjwa waliopelekwa nje ya nchi kwa gharama za Serikali kutoka wagonjwa 423 mwaka 2015 na hadi kufikia wagonjwa 203 mwezi Oktoba 2017. Mafanikio haya ni kutokana na maboresho mbalimbali yaliyofanywa katika Hospitali za Kitaifa za Serikali.

Hospitali za Taifa Muhimbili (MNH)

·       Serikali imeiwezesha Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kufanya maboresho mbalimbali ikiwa ni pamoja na;-
-         Ununuzi wa Vifaa Tiba vya Kisasa kama CT-Scan iliyofungwa katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili.
-         Kuongeza Vitanda vya Wagonjwa Mahututi (ICU) kutoka 21 mwaka 2015 na kufikia 74 mwaka 2016/2017
-         Kuongeza vyumba vya upasuaji kutoka 13 mwaka 2015 na kufikia 20 mwaka 2017 na hivyo kupunguza muda wa wagonjwa kusubiri kutoka miaka 2 hadi miezi 4 au 6 .
-         Kujenga Vyumba 2 vya upasuaji kwa watoto ambapo sasa upasuaji unafanywa kwa watoto 50 kwa wiki kutoka watoto 15 kwa wiki mwaka 2015 na hivyo kupunguza muda wa watoto kusubiri upasuaji kutoka miaka 2 hadi miezi 4.
-         Mashine kwa ajili ya kusafisha damu kwa wagonjwa wa figo (dialysis) zimeongezeka kutoka 27 mwaka 2015 hadi kufikia 42 na hivyo kupunguza muda na mrundikano wa wagonjwa wanaohitaji huduma za kusafisha damu nchini
-         Kuanzisha Huduma za kupandikiza vifaa vya kuongeza usikivu (Cochlear implant) na hivyo kuwezesha watoto waliozaliwa na matatizo ya usikivu kupata huduma hizi kwa gharama ya shilingi milioni 34 kwa mtoto badala ya shilingi milioni 80 iwapo wangepelekwa kupata huduma hii nje ya nchi. Vilevile MNH iko mbioni kuanza huduma za upandikizaji figo kabla ya mwisho wa mwezi Desemba 2017.
https://fullshangweblog.com/home/wp-content/uploads/2017/10/Picha-no.-3.jpg

Madaktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu katika Taasisi ya Jakaya Kikwete (JKCI) wakimfanyia mgonjwa upasuaji



UPASUAJI WA MOYO

·       Huduma za Upasuaji wa Moyo nchini kupitia Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) zimeboreshwa. Hivi sasa JKCI ina uwezo wa kupasua  wagonjwa 3 kwa siku sawa na wagonjwa 90 kwa mwezi ikilinganishwa na kupasua mgonjwa 1 kwa siku ,sawa  na wagonjwa 15 kwa mwezi tangu kuanzishwa Taasisi hiyo mwaka 2016. Hivyo  fedha nyingi ambazo zingetumika kupeleka wagonjwa nje ya nchi zimeokolewa na ujuzi wa Wataalam wetu umezidi kuimarika. Aidha JKCI imeanza kupokea wagonjwa kwa ajili ya upasuaji wa moyo kutoka nchi jirani ikiwemo Malawi,Kenya, Burundi, Uganda, Comoro, DRC, Rwanda na Zambia.

MATIBABU YA SARATANI

·       Kuhusu matibabu ya Saratani Taasisi ya Saratani ya Ocean Road (ORCI), Serikali imeongeza vitanda na vifaa vya kuwahudumia wagonjwa wanaopata tiba ya saratani kwa njia ya dawa (Chemotherapy) kutoka wagonjwa 40 mwaka 2015 hadi 100 mwaka 2017. Taasisi imepunguza muda wa wagonjwa kusubiri kuanza tiba ya Mionzi (Radiotherapy) kutoka miezi 3 hadi wiki 6. Muda huo utaendelea kupungua hadi kufikia wiki 2.

Upatikanaji wa dawa za saratani umeboreshwa kutoka asilimia 4 mwaka 2015/16 hadi kufikia asilimia 80 mwezi Oktoba 2017, na kwa baadhi ya saratani kama ya mlango wa kizazi, saratani ya koo na tezi dume dawa za dripu (chemotherapy) zinapatikana kwa asilimia 100.

KUONGEZEKA KWA WANANCHI WALIOJIUNGA NA MIFUKO YA BIMA YA AFYA

·       Kupitia azma ya Serikali ya Awamu ya Tano ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma za afya bila kikwazo cha fedha, hatua mbalimbali zimechukuliwa ikiwemo kuhamasisha wananchi juu ya umuhimu wa kuwa na uhakika wa matibabu kabla ya kuugua. Hatua hii imewezesha  kuongezeka kwa idadi ya Watanzania waliojiunga na Mifuko ya Bima ya Afya kutoka 27% mwaka 2015/16 hadi 31.5% Septemba 2017 sawa na wananchi wapatao 15,675,396.

HUDUMA ZA AFYA YA MAMA NA MTOTO ZABORESHWA ZAIDI

·       Huduma za Afya ya Uzazi, Mama na Mtoto zimeboreshwa ambapo Serikali inanunua, kusambaza na kutoa bila malipo dawa kwa ajili ya uzazi salama kwa wanawake wote wajawazito wanaofika katika vituo vya kutolea huduma vya Serikali ikiwemo dawa kwa ajili ya kuongeza damu (Fefol), dawa ya kuzuia kutokwa na damu baada ya kujifungua (Oxytocin), pamoja na dawa kwa ajili ya kifafa cha mimba (Magnesium Sulphate). Pia, Serikali imegawa magari ya kubebea wagonjwa (Ambulance) 67 aina ya Land Cruiser katika Halmashauri za Mikoa yote ya Kanda ya Ziwa na Kigoma na Mikoa mingine hapa nchini ili kuimarisha huduma za rufaa kwa wagonjwa hasa wanawake wajawazito.

·       Ili kuokoa maisha ya mama na mtoto mchanga, Serikali ya awamu ya tano inaanzisha ujenzi wa miundombinu muhimu kwa ajili ya kutoa huduma za uzazi za dharura ikiwemo upasuaji wa kumtoa mtoto tumboni ambapo  vyumba vya upasuaji (Theatres) vipatavyo 170 vinajengwa katika Vituo mbalimbali vya Afya nchini. Kukamilika kwa mpango huu kutaongeza idadi ya vituo vya Afya vya Serikali (Health Centres) vinavyotoa Huduma za uzazi za Dharura ikiwemo upasuaji kutoka 109 ya mwaka 2016 na kufikia 279 mwaka 2017 na hivyo kuokoa maisha ya mama na mtoto mchanga.

KUPANUA WIGO WA UPATIKANAJI WA DAWA ZA ARV NA MATIBABU YA KIFUA KIKUU

·       Kuanzia mwezi Oktoba 2016, Serikali imeanza kutoa dawa za ARV kwa watu wenye maambukizi ya Virusi vya VVU/UKIMWI (WAVIU) bila kujali kiwango cha CD4 ambapo hadi kufikia Oktoba 2017, jumla ya WAVIU wanaotumia ARV/ART ni  935,228 zilizokuwa zikitolewa katika vituo vya huduma za tiba na matunzo vipatavyo 6,259 nchi nzima. Idadi hii ni sawa na asilimia 67 tu ya watu 1,400,000 wanaokadiriwa kuwa na maambukizi ya VVU nchini.
·       kuanzia Desemba 2016, Serikali imeimarisha na kusogeza huduma za uchunguzi na matibabu ya kifua kikuu sugu karibu na wananchi kutoka Hospitali moja ya Kibongoto  (Kilimanjaro) mwaka 2015 hadi Vituo 18 vilivyoko katika mikoa 9 ya Geita, Dar es salaam, Mtwara, Morogoro, Pwani, Mbeya, Kagera, Tanga na Simiyu

VITANDA VYA WAGONJWA NA MASHUKA VYASAMBAZWA NCHI NZIMA

Ili kutimiza ahadi ya Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ya kuhakikisha kila kituo cha kutolea huduma za afya cha Umma kinakuwa na vifaa vya kutosha, Serikali imenunua na kusambaza kwa kila Halmashauri vitanda vya Hospitali 20, vitanda vya kujifungulia 5, magodoro 25 na mashuka 50. Jumla ya vitanda vya Hospitali vya kawaida (Hospital beds) 3,680, vitanda vya kujifungulia (delivery beds) 920, magodoro 4,600 na mashuka 9,200 vimenunuliwa na kusambazwa.

Waziri,Naibu Waziri,Menejimenti pamoja na Watumishi wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto tunashukuru na kukupongeza Rais wetu Mpendwa kwa Juhudi zako za dhati katika kuboresha huduma za Sekta ya afya nchini

 Tutaendelea kutekeleza”


Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement