Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile aliyevaa shati la vyumbavyumba akikagua na kutoa maelekezo juu ya upatikanaji wa dawa katika baadhi ya vituo vya afya katika Wilaya ya Meru wakati wa ziara yake mkoani Arusha.

Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati akipata maelezo kutoka kwa mmoja ya  mtumishi wa  Chuo Cha Maendeleo ya Jamii cha Tengeru (TICD) wakati alipotembelea chuo hiko katika ziara yake mkoani arusha.

Baadhi ya Watumishi wa Chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru TICD wakimsikiliza kwa makini Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile hayupo pichani wakati alipotembelea chuo hiko katika ziara yake mkoani Arusha.

Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile katikati akionyeshwa mpaka  wa Chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru TICD wakati alipotembelea chuo hiko katika ziara yake mkoani Arusha.

Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile aliyevaa shati la vyumbavyumba akiwajulia hali baadhi ya wagonjwa  katika vituo vya afya katika Wilaya ya Meru wakati wa ziara yake mkoani Arusha.

Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile wa pili kulia akisikiliza maelezo kutoka kwa Mganga Mkuu wa Wilaya ya Meru Dkt. Cosmas Kilasara wa kwanza kulia kwenye moja ya jengo la Hospitali ya Wilaya ya Meru mkoani Arusha.

Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile kulia akiongea na baadhi ya wanakijiji wa kata ya Mbuguni wilayani Meru wakati wa ziara yake mkoani Arusha.

Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru TICD wakitoa chngamoto na maswali kwa Naibu Waziri Wa afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia ,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile hayupo pichani wakati alipotembelea chuo hiko katika ziara yake mkoani Arusha.


Na WAMJW- ARUSHA.
NAIBU Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile amutaka uongozi wa Chuo Cha Maendeleo ya Jamii Tengeru kuunda Bodi ya chuo haraka iwezekenavyo ili kuleta maendeleo ya kitaaluma chuoni hapo.

Hayo ameyasema wakati alipotembelea Chuo hiko leo katika ziara yake ya siku mbili mkoani Arusha kwa ajili ya kuangalia hali ya upatikanaji wa huduma za afya .

"Uongozi wa chuo unatakiwa kuhakikisha unakuwa na bodi ya chuo pamoja na kuwa na Mkuu wa chuo alithibitishwa kwani mpaka sasa hakuna mkuu wa chuo hiyo ni hatari"alisema Dkt. Ndugulile

Aidha Dkt. Ndugulile amesema kuwa uongozi wa chuo hiko hauna budi kuhakikisha unamaliza tatizo la mipaka na kupata hati miliki ya kiwanja hiko kwani inaweza kusababisha upokwaji wa kiwanja hiko.

Katika ziara hiyo Dkt. Ndugulile alifanikiwa kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Meru na kujiridhisha na hali ya upatikanaji wa dawa na kuwasisitiza wananchi wasiuziwe dawa zote muhimu.

Aidha Dkt. Ndugulile ametembelea Kituo cha Afya Mbuguni na kuwapongeza kutokana na kupeana elimu juu ya uzazi wa mpango kwa wanakijiji wote wa kata hiyo na kufanya kupata huduma za afya kwa urahisi na kwa ufasaha.

"Ila nataka niwaambie wanakijiji hata kama dawa zipo kwa asilimia 100 na sisi ni lazima tujikinge na magonjwa yasioambukiza kwani yamekuwa tishio kwa watanzania"alisema Dkt. Ndugulile 

Aidha Dkt. Ndugulile amepongeza viongozi wa Hospitali ya Meru na Kituo cha afya Mbuguni Wilayani Meru kwa kupiga hatua katika kutokomeza vifo vya mama na watoto.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement