Dk. Tulia (mwenye miwani),Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Watoto wa JKCI, Sulende Kubhoja, Mkurugenzi wa DSTV Maharage Chande(mwenye koti na tai) na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utawala na Fedha, Agnes Kuhenga wakionesha waandishi wa habari moja ya televisheni ambazo zimetolewa na Taasisi ya Tulia Trust kwa ajili ya wodi za watoto JKCI.
Na Mwandishi Maalum, Dar es Salaam
Naibu spika
wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Tulia Ackson amekabidhi msaada
wa televisheni kwa Taasisi hiyo ambazo zitafungwa katika wodi za watoto.
Akizungumza na
waandishi wa habari jana Dkt. Tulia alisema ametoa jumla ya televisheni sita
kwa JKCI kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wakiwamo kampuni ya DSTV.
“Kwa mara ya
kwanza niliguswa kutoa msaada huu wa televisheni nilipokuja kumuona mtoto ambaye
taasisi ya Tulia Trust imegharamia matibabu yake.
“Hadi sasa
tumetoa jumla ya televisheni sita zenye jumla ya thamani ya Sh milioni 20,”
alisema.
Naibu Spika
huyo alisema taasisi ya Tulia Trust inajihusisha na uboreshaji wa huduma
mbalimbali za kijamii hasa elimu, afya na miundombinu.
Dk. Tulia akifurahia zawadi ya kalenda aliyokabidhiwa na Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utawala na Fedha, Agnes Kuhenga (mwenye koti) ni Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo wa Watoto wa JKCI, Sulende Kubhoja (mwenye koti na tai) ni Mkurugenzi wa DSTV Maharage Chande.
“Huwa tunapokea
maombi kutoka kwa watu mbalimbali wenye
uhitaji ambao wengi huja moja kwa moja kwetu, tunatoa misaada hiyo kwa
kushirikiana na wadau,” alisema.
Alisema kupitia
taasisi hiyo wanakusudia kuzisaidia hospitali nyingi zaidi kuanzia za mikoa,
tarafa na zile zinazotoa huduma kwa watoto.
Dk. Tulia akizungumza na baadhi ya wazazi wenye watoto wanaotibiwa magonjwa ya moyo katika taasisi hiyo mapema leo.
“Tutafanikisha
hilo kwa kushirikiana na wadau wetu na tayari wameitikia suala hilo, huwa
tunasaidia kujenga vyumba vya upasuaji,
kugawa mifuko ya sementi, mabati, vitanda na vifaa tiba,” alisema.
Kwa upande
wa Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo
kwa Watoto wa JKCI, Sulende Kubhoja (pichani) aliishukuru taasisi hiyo kwa kukabidhi msaada huo.
“Televisheni
hizi naamini zitasaidia kuwafariji na kuwaondolea upweke watoto wanaolazwa
wodini wakati wakisubiri huduma,” alisema.
Kaimu Mkurugenzi Idara ya Utawala na Fedha, Agnes Kuhenga amewaomba wadau wengine kuiga mfano wa Tulia Trust.
Dk. Tulia akiwa amembeba mmoja wa watoto wanaotibiwa moyo katika taasisi ya JKCI.
Picha zote na Veronica Romwald
Chapisha Maoni