Kaimu Mkurugenzi wa Idara ya Magonjwa ya Moyo wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Peter Kisenge akisoma taarifa za utendaji kazi wa idara yake kwa kipindi cha miezi mitatu katika kikao cha kwanza cha Menejimentikwa mwaka 2018 kilichofanyika hivi karibuni.
Na Mwandishi Wetu,
Na Mwandishi Wetu,
Uongozi wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) umeahidi kuendelea kutoa huduma bora za matibabu kwa kiwango cha kimataifa kwa wagonjwa wanaosumbuliwa na magonjwa ya
moyo wanaotibiwa katika Taasisi hiyo.
Ahadi
hiyo imetolewa hivi karibuni na Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof.
Mohamed Janabi alipozungumza na wakurugenzi wa Idara na vitengo vinavyojitegemea
katika kikao cha kwanza cha Menejimenti kwa mwaka 2018.
Prof. Janabi (mwenye koti jeupe) ambaye pia ni Mwenyekiti wa kikao hicho alizitaja
ahadi zingine ni pamoja na kuendeea kupunguza kupeleka wagonja nje ya nchi,
kupunguza gharama za tiba, kuongeza idadi ya huduma, kuboresha usafi katika
Hospitali na kuendelea kushirikiana na
wananchi.
Kikao cha kwanza cha Manejimenti cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa mwaka 2018 kikiendelea.
“Malengo tuliyokuwa nayo kwa mwaka huu wa 2018 ni kuona wagonjwa wengi zaidi ya hawa tuliowaona mwaka 2017 katika kliniki zetu za kila siku. Taasisi imejipanga kufanya upasuaji wa kufungua kifua kwa wagonjwa 400 na bila kufungua kifua kwa wagonjwa 1000.Tunatarajia kuwa na kambi maalum za upasuaji wa moyo zisizozidi 15”.
“Malengo tuliyokuwa nayo kwa mwaka huu wa 2018 ni kuona wagonjwa wengi zaidi ya hawa tuliowaona mwaka 2017 katika kliniki zetu za kila siku. Taasisi imejipanga kufanya upasuaji wa kufungua kifua kwa wagonjwa 400 na bila kufungua kifua kwa wagonjwa 1000.Tunatarajia kuwa na kambi maalum za upasuaji wa moyo zisizozidi 15”.
“Mwezi huu tunatarajia kuwa na kambi mbili
zote ni za upasuaji wa bila kufungua kifua. Tunaanza na kambi ya watu wazima kwa kushirikiana na Taasisi
ya Madaktari Afrika ya nchini Marekani. Mwisho wa mwezi tutakuwa na kambi ya watoto kwa kushirikiana
na Taasisi ya Okoa Moyo wa Mtoto (Save a Child’s Heart-SACH) ya nchini Israel”,
alisema.
Wakurugenzi wa Idara na vitengo vinavyojitegemea vya Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) wakimsikiliza Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi hiyo Prof. Mohamed Janabi (hayupo pichani)
Kwa upande wa viongozi waliohudhuria mkutano huo Prof. Janabi aliwataka kuwasimamia wafanyakazi wanaowaongoza ili waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi na uweledi huku wakifuata maadili ya watumishi wa Umma hii itawafanya wananchi waweze kupata huduma bora zaidi.
Nao
viongozi waliohudhuria mkutano huo walisema kuwa watahakikisha wanafanya kazi
zao kwa kujituma, kufuata kanuni za kazi na kuwasimamia wafanyakazi wanaowaongoza ili
wananchi waweze kunufaika na matibabu ya moyo yanayotolewa katika Taasisi hiyo.
Kikao kikiendelea
Kwa mwaka 2017 jumla ya wagonjwa 1025 walifanyiwa upasuaji wa kufungua kifua na bila kufungua kifua katika Taasisi hiyo ambapo zaidi ya bilioni 29 (Tshs. 29,725,000,000/=) ziliweza kuokolewa kama wagonjwa hao wangetibiwa nje ya nchi. Gharama za mgonjwa mmoja anayetibiwa nje ya nchi ugonjwa wa moyo ni zaidi ya milioni 29.
Kwa mwaka 2017 jumla ya wagonjwa 1025 walifanyiwa upasuaji wa kufungua kifua na bila kufungua kifua katika Taasisi hiyo ambapo zaidi ya bilioni 29 (Tshs. 29,725,000,000/=) ziliweza kuokolewa kama wagonjwa hao wangetibiwa nje ya nchi. Gharama za mgonjwa mmoja anayetibiwa nje ya nchi ugonjwa wa moyo ni zaidi ya milioni 29.
Chapisha Maoni