Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

KILIO cha muda mrefu cha Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), kuhusu ufinyu wa nafasi ya kulaza wagonjwa hasa watoto wenye matatizo ya moyo, hatimaye kimesikika na kuanza kufanyiwa kazi.

mapema wiki iliyopita kupitia taarifa yake kwa umma iliyotolewa na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano ya Umma na Masoko, Anna Nkinda taasisi hiyo ilieleza inakabiliwa na ufinyu wa nafasi kwa Chumba cha Wagonjwa Mahututi na nafasi ya kulaza wagonjwa hasa watoto.

Mapema wiki hii, Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu ameipatia JKCI nafasi ya kuweka vitanda 50 vya wagonjwa.

Uamuzi huo ulitolewa hivi karibuni na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu, alipofanya ziara ya kushtukiza Muhimbili.

Ziara hiyo ililenga kukagua utekelezaji wa agizo alilotoa hivi karibuni kwa hospitali hiyo kuhamisha wagonjwa na Idara yote ya Magonjwa ya ndani kwenda Mloganzila.

Waziri Ummy aliuagiza uongozi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kuipatia JKCI nafasi hiyo katika jengo la watoto.


"Nimekuja kukagua iwapo agizo nililotoa limetekelezwa, nimefurahi kwamba limetekelezwa na tayari baadhi ya wagonjwa na madaktari 15 na wauguzi zaidi ya 30 wamehamia Mloganzila," alisema na kuongeza

"Kwa hatua hiyo tunakuwa na nafasi pale wodi ya Mwaisela na hapa jengo la watoto," alisema.

Alisema kwa kuwa JKCI inafanya kazi nzuri ya kutibu magonjwa ya Moyo lakini wanakabiliwa na uhaba wa vitanda kwa sababu hawana nafasi Muhimbili ihakikishe inapa nafasi ya kuweka vitanda 50 vya kulaza wagonjwa ndani ya Jengo la Watoto.

Alisema hiyo itawezesha Taasisi hiyo kukabiliana na changamoto hiyo iliyopo hivi sasa.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement