Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiW7UqcadNpHBmsOHxH0Y0IL6Av5VGugTzXMhqDvBKvq8CSzLK5wzqAWYqy2W5sNauNAWElgWv1nhjNzkTXerWuxM-4ot5rLjdQ-I-FNquNT5H7SX0yt-6CB50-TJ9EcCA9cXCWmCPO0eo/s640/pesa.jpgNa Veronica Romwald, Dar es Salaam
Serikali inakusudia kuanza kununua dawa za kuhifadhia maiti moja kwa moja kutoka kwa wazalishaji viwandani.

Hatua hiyo itachukuliwa ili kusaidia kuwapunguzia wananchi mzigo wa gharama ya kuhifadhi maiti katika hospitali mbalimbali.

Kauli hiyo ilitolewa Dar es Salaam le na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu wakati wa ziara yake aliyofanya katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Amana.

Katika Hospitali hiyo wananchi hulipia kiasi cha Sh 30, 000 kwa siku ikiwa ni gharama za kuhifadhiwa miili ya ndugu na jamaa zao waliofariki dunia.

"Changamoto hii ipo katika maeneo mengi nchini, hivyo tunakusudia kuanza kununua dawa hizi moja kwa moja kwa wazalishaji na kisha tutatoa bei elekezi kwa ajili ya kumpunguzia gharama mwananchi," amesema.

Awali alisema anaridhishwa na utendaji kazi hospitalini hapo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement