Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam

TAASISI ya Saratani Ocean Road itapatiwa kiasi cha Sh bilioni 14.5 katika mwaka ujao wa fedha ili iweze kununua mashine ya kisasa ya Pet Scan yenye uwezo wa kutibu magonjwa ya saratani.

Hayo yalielezwa Dar es Salaam jana na Naibu Waziri wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Faustine Ndugulile alipofanya ziara katika Taasisi hiyo.

“Nimeridhika huduma ni nzuri wanazotoa, tunakusudia katika mwaka ujao wa fedha kuwaongezea bajeti, ttutawapa kiasi hicho cha fedha ili wanunue mashine hiyo kusudi matibabu ya kibingwa dhidi ya magonjwa ya saratani yapatikane hapa hapa nchini,” alisema.

Alisema tayari hospitali hiyo ilipatiwa fedha imenunua mashine ya CT simulator Linac ambayo nayo inatibu kwa kiwango cha kisasa na kibingwa magonjwa ya saratani.

“Tuliwapatia zaidi ya Sh. bilioni 9.5 kununua mashine hiyo, hatua hii inaifanya Tanzania kuwa nchi ya kwanza Barani Afrika kuwa na mashine hiyo yenye uwezo wa juu katika kutibu magonjwa ya saratani,” alisema.

Aliongeza “Tunataka ifikapo April, mwaka huu mitambo hii iwe imekamilika ili ianze kutoa huduma, nimeridhika pia na hali ya majengo wamejitahidi mno vile vile hali ya upatikanaji dawa ni nzuri.

“Lakini kwa upande wa tiba ya mionzi kuna changamoto, mashine moja imeharibika na wamesema kifaa kimefika, nimeagiza ndani ya wiki hii itengenezwe ili ifanye kazi kuondoa msongamano uliopo wa wagonjwa,” alisema.

Aliwataka ORCI kukusanya takwimu za wagonjwa wa saratani nchi nzima ili serikali iweze kujua idadi yao, wapi walipo na aina gani ya satatani wanaugua.

“Tunataka tuwatambue hiyo itatusaidi serikali tuwe thabiti kuweza kuwahudumia wagonjwa hawa,” amesisitiza.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa ORCI, Dk. Julius Mwaiselage alisema hivi sasa mafundi wa taasisi hiyo wanaendelea na shughuli ya ufungaji mashine hiyo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement