Madaktari wa JKCI wakimfanyia mgonjwa upasuaji (picha na mtandao)
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
WAGONJWA 19,371 WATIBIWA KATIKA TAASISI YA MOYO JAKAYA KIKWETE
KUTOKA JANUARI HADI MACHI 2018.
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI)
kwa kipindi cha miezi mitatu ya Januari hadi Machi 2018 imeona jumla ya
wagonjwa 19,371 wenye matatizo mbalimbali ya moyo kati ya hao wagonjwa wa nje
ni 18,481 na waliolazwa ni 890.
Wagonjwa 105 walifanyiwa upasuaji wa
moyo wa kufungua kifua kati ya hao watu wazima 53 na watoto 52. Kati
ya wagonjwa 105 waliofanyiwa upasuaji 66 walifanyiwa na
madaktari wetu bingwa wa magonjwa ya moyo watoto wakiwa
ni 35 na watu wazima 31.
Upasuaji wa moyo bila kufungua kifua (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab ulifanyika kwa wagonjwa 231 kati ya hao watoto ni 20 na wakubwa 211. Kati ya wagonjwa 231 waliotibiwa wagonjwa watu wazima 211 walifanyiwa upasuaji na madaktari wetu wa ndani.
Upasuaji wa moyo bila kufungua kifua (Catheterization) kwa kutumia mtambo wa Cathlab ulifanyika kwa wagonjwa 231 kati ya hao watoto ni 20 na wakubwa 211. Kati ya wagonjwa 231 waliotibiwa wagonjwa watu wazima 211 walifanyiwa upasuaji na madaktari wetu wa ndani.
Kwa kipindi cha miezi mitatu
tumekuwa na jumla ya kambi za matibabu nane (8) ambapo tulifanya
matibabu kwa kushirikiana na washirika wetu kutoka nchi za Ujerumani, Israel,
Australia , Marekani, India na Falme za Kiarabu. Katika kambi hizo jumla ya
wagonjwa 39 walifanyiwa upasuaji wa kufungua kifua kati ya hao watoto 17 na
watu wazima 22. Wagonjwa 72 walifanyiwa upasuaji wa bila kufungua kifua
kati ya hao watoto 20 na watu wazima 52.
Tumefanya upasuaji wa
kuunganisha mishipa ya damu (AVF- Arterio Venous Fistula) kwa ajili ya
kusafishia damu kwa wagonjwa wenye matatizo ya figo (Hemodialysis) 36.
Changamoto kubwa tunayokabiliana nayo
ni wagonjwa wengi tunaowapokea mioyo yao kutokuwa katika hali nzuri hivyo basi
tunawaomba wananchi kujenga tabia ya kupima afya zao mara kwa mara
hii itawasaidia kujuwa kama wana matatizo ya moyo au la na kama
wanamatatizo wataweza kupata tiba kwa wakati.
Wazazi na walezi tunawaomba wasisahau
kupima afya za watoto wao pale watakapoona kuna hali ya tofauti katika ukuaji
wa mtoto kwani magonjwa mengi ya moyo yanaanzia utotoni. Mtoto akianza kuuguwa
magonjwa ya moyo wazazi wengi wanadhani ni matatizo ya kifua baada ya kumfikisha
Hospitali na kufanyiwa vipimo ndipo inagundulika mtoto anasumbuliwa
na magonjwa ya moyo. Kwa wamama wajawazito wafanye uchunguzi (Fetal
Echocardiography) wa kuangalia kama mtoto aliyeko tumboni anamatatizo ya moyo.
Aidha kwa upande wa gharama za matibabu
Taasisi yetu imeyagawa katika makundi manne (4) tuna wagonjwa
wanaotibiwa kwa bima mbalimbali ambazo tumeingia makataba nazo. Wagonjwa
wanaolipia gharama zote wenyewe, wagonjwa wanaochangia kidogo huku
gharama zingine zikilipwa na Serikali. Kundi la mwisho ni wagonjwa
ambao hawalipii kabisa gharama za matibabu ikiwa watakidhi vigezo
vyote vya kutokulipa.
Huduma zetu za matibabu ya
moyo zinatolewa kwa watanzania wote wa Bara na Visiwani. Ifahamike
kwamba fedha za matibabu zinazolipwa na wagonjwa zinatumika kununua
vifaa tiba vya moyo kama mlango wa moyo (Valve), betri ya moyo
(Pacemaker) na vinginevyo.
Kutokana na matibabu ya moyo kuwa ya
gharama kubwa tunaendelea kuwasisitiza wananchi wajiunge na mifuko ya bima za
afya ambayo itawasaidia kulipa gharama za matibabu pindi watakapohitaji
kutibiwa. Pia itasaidia Hospitali yetu kuendelea kujiendesha yenyewe kwa
kushirikiana na Serikali na wadau wengine.
Imetolewa na:
Kitengo cha Uhusiano
Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete
19/04/2018
Chapisha Maoni