WIZARA YA AFYA, MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WAZEE NA WATOTO
TAARIFA KWA UMMA
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, inapenda kuufahamisha Umma kuwa, Awamu ya Kwanza ya Watumishi wa Wizara kuhamia Makao Makuu ya Nchi, Mkoani Dodoma imetekelezwa tarehe 23 Februari, 2017.
Miongoni mwa waliohamia Dodoma katika awamu hii ya kwanza ni Viongozi na Watendaji Wakuu wa Wizara wakiongozwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu, Naibu Waziri Mhe. Dk. Hamis Kigwangalla.
Wengine ni Makatibu Wakuu wa Wizara Idara kuu ya Afya na Idara kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia Wazee na Watoto.
Kufuatia Uhamisho huo, jumla ya watumishi 90 wa Wizara hiyo wameungana na viongozi wao kuitikia uhamisho huo.
Anwani za Wizara zitakazotumika mkoani Dodoma ni kama ifuatavyo:
Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Idara Kuu ya Afya,
Chuo Kikuu Dodoma,
Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Maendeleo ya Jamii,
S.L.P 743,
Jengo Namba 11,
DODOMA.
Namba ya Simu +255 26 2323267
Anwani nyingine
Katibu Mkuu,
Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Idara Kuu ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto,
Chuo Kikuu Dodoma,
Kitivo cha Sanaa na Sayansi ya Maendeleo ya Jamii,
S.L.P 573,
Jengo Namba 11
DODOMA.
Imetolewa na;
KATIBU MKUU
WIZARA YA AFYA MAENDELEO YA JAMII JINSIA WAZEE NA WATOTO
24/2/2017
Chapisha Maoni