Na Mwandishi Maalum
Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania (TMDA), Kanda ya Kusini, baada ya kuwekeza katika taarifa za kiintelijensia Januari 30, 2021 ilifanikiwa kutega mtego Wilaya ya Newala Mji na kumnasa, Jamaly Sadick akiuza dawa za Serikali za Mpango wa Uzazi.
Meneja Uhusiano kwa Umma wa TMDA, Gaudensia Simwaza amesema dawa hizo ni Medroxy Progesterone (vichupa 60) na Microgynon pills (vidonge 3360) zote zikiwa na thamani ya Tshs 300,000/-
Amesema mtuhumiwa na mtoto wake wamefunguliwa jalada polisi RB No.NL/RB/94/221 na yuko ndani kwa hatua zaidi kisheria.
Chapisha Maoni