Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Mzigo wa gharama za usafiri kwa mwananchi kufuata huduma za matibabu dhidi ya Homa ya Ini kutoka maeneo mbalimbali ya nchi hadi Hospitali ya Taifa Muhimbili {MNH}, utapungua Tanzania.

Ahueni hiyo inatarajiwa kwani Serikali kupitia Wizara ya Afya tayari imekamilisha mwongozo  wa matibabu ya Homa ya Ini.

Mwongozo huo utatumika kutoa maelekezo ya tiba hiyo nchi nzima ili kumpunguzia mwananchi gharama ya kusafiri umbali mrefu kwenda kupata tiba hiyo, Muhimbili.

Waziri wa Afya, Ummy Mwalimu amebainisha hayo wakati alipotoa tamko lake kwa umma leo ikiwa ni Siku ya Homa ya Ini Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka julai 28.

Waziri Ummy ameeleza hatua nyingine nyingine zinazotekelezwa na Serikali kupambana na ugonjwa huo.

“Katika kuendelea kudhibiti homa hii, Wizara pia itaendelea kusimamia Mpango Mkakati wa Taifa wa Kudhibiti na Kutomeza Ugonjwa wa Homa ya Ini nchini wa mwaka 2018-2023.

Amesema Wizara inaendelea kuaandaa vielelezo vinavyohusu ugonjwa huo {Viral Hepatitis}, ili kuuelimisha umma hususan namna gani maambukizi yanaweza kuzuiwa.

Amesema Wizara inaendelea kutoa elimu ya ugonjwa huo kupitia vyombo vya habari pia.

“Utaratibu wa kuwapatia mama wajawazito kinga ya kuzuia maambukizi ya Homa ya Ini aina B kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto zipo katika hatua za mwisho,” amesema nao unaendelea.

Ameongeza “Tunaendelea na mchakato wa kuunganisha huduma ya homa ya Ini na mpango wa taifa wa kudhibiti UKIMWI nchini, ili iwe rahisi kuwekea mikakati ya kudhibiti ugonjwa huu.

Amesema ripoti ya Homa ya Ini ya mwaka 2021 ya Shirika la Afya Duniani {WHO} zinaeeleza mwaka 2019 watu 296 duniani waligundulika wanaishi na Homa sugu ya Ini kirusi aina B.

Amesema takwimu zinaeleza zaidi ya nusu {66%} ya maambukizi hayo yalitoka Bara la Afrika huku watu wapatao milioni 58 walikuwa wanaishi na maambukizi ya Homa ya Ini kisuri aina C.

Ameongeza “.., na wakati huo huo kulikuwa na vifo 820,000 duniani vilivyosababishwa na Homa ya Ini kirusi aina B.

“Kwa Tanzania, takwimu kutoka Mpango wa Taifa wa Damu Salama (NBTS) zinaonesha kuwa maambukizi ya Homa ya Ini aina ya B miongoni mwa wachangiaji damu kwa miaka mitatu ni kama ifuatavyo mwaka 2018 (4.4%), mwaka 2019 (5.9), mwaka 2020 (6.1%) na mwaka 2021 (5.3%).

“Aidha, kwa kipindi hicho maambukizi ya Homa ya Ini aina C yameendelea kuwa ni ya 2.3%,” amebainisha.

Amesema Ugonjwa wa Ini aina ya A na E unaweza kuzuilika kwa kuboresha usafi wa mazingira, utayarishaji wa vyakula katika hali ya usafi na matumizi ya maji safi na salama.

Amesema Ugonjwa wa Homa ya Ini aina ya B, C na D inazuilika kwa kutekeleza afua zote za kuzuia virus vya VVU/UKIMWI.

Amehimiza wananchi kuchukua tahadhari ikiwa ni pamoja na kupata chanjo dhidi ya ugonjwa huu kwa wale ambao hawajawahi kuipata kwani zinatolewa nchini Tanzania, akibainisha kwamba tangu mwaka 2002 watoto wamekuwa wakipatiwa chanjo hiyo.

“Niwasisitize wadau wote katika sekta binafsi na umma kuendelea kuona umuhimu na kutoa kipaumbele na kuwekeza katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa Homa ya Ini nchini na hatimaye kuweza kuutokomeza kabisa ifikapo mwaka 2030,” ametoa rai.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement