Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Dodoma

Idadi ya bidhaa za dawa, vifaa tiba na vitendanishi vinavyosajiliwa nchini imeongezeka ndani ya kipindi cha mwaka 2021/22 katika Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba Tanzania {TMDA}.

Yameelezwa hayo leo Jijini hapa na Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Adam Fimbo alipotoa taarifa ya mafanikio ya Taasisi hiyo katika kipindi hicho, mbele ya waandishi wa habari, amesema jumla ya bidhaa 1,286 zimesajiliwa.

kati yake bidhaa za dawa za binadamu na mifugo ni 933 na vifaa tiba na vitendanishi ni 353,” amebainisha.

Fimbo ameongeza “Kwa idadi hii jumla ya bidhaa zilizosajiliwa hadi sasa imefikia 8,831 ambapo kati yake bidhaa za dawa ni 6674 na vifaa tiba na vitendanishi ni 2,157.

“Hii inaashiria kiasi kikubwa cha dawa zinazotumika Tanzania zimehakikiwa na hivyo ni bora, salama na fanisi kwa matumizi ya binadamu,” amesisitiza.

Kuhusu usajili wa majengo na ukaguzi, amesema katika kipindi hicho TMDA imesajili jumla ya maeneo 467 yanayojihusisha na biashara za bidhaa zinazodhibitiwa kwa lengo la kuhakikisha kuwa maeneo husika yanakidhi vigezo ili kutoathiri ubora, usalama na ufanisi wa bidhaa.

“Aidha, jumla ya maeneo 10,938 yanayojihusisha na biashara ya dawa, chanjo, vifaa tiba na vitendanishi yalikaguliwa kwa mwaka 2021/22 ikiwa ni ongezeko la maeneo 92 yaliyokaguliwa ikilinganishwa na maeneo 10,846 yaliyokaguliwa mwaka 2020/21.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement