Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Siku chache zikiwa zimesalia kufikia matembezi ya hisani [MEWATA WOGGING], Waziri wa Afya Ummy Mwalimu ameweka wazi kwamba atashiriki ipasavyo kwani yana nia njema ya kujenga jamii yenye afya bora.

Akizungumza mapema leo baada ya kuhitimika kwa matembezi ya hisani [Walk the Talk] ya Shirika la Afya Duniani [WHO  Tanzania], Waziri Ummy amesisitiza, yupo tayari kushiriki matembezi yoyote ili kuhimiza jamii kujenga desturi ya mtindo bora wa maisha.

MEWATA WOGGING imeandaliwa na Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania [MEWATA] April 20, 2024 inatarajiwa kufanyika huko Mbweni JKT - Dar es Salaam.

Lengo ni kuzidi kuhimiza mtindo bora wa maisha na kukusanya fedha kwa ajili ya ujenzi wa hospitali kubwa ya kuhudumia jamii.

Waziri Ummy amesema pamoja na Serikali kuzingatia katika kuimarisha miundombinu ikiwamo ujenzi wa zahanati, vituo vya afya na hospitali, ununuzi vifaa tiba na upatikanaji wa dawa,
Lakini pia imedhamiria kuwekeza katika afua za kinga ili kuilinda na kuikinga jamii dhidi ya magonjwa yasiyoambukiza ambayo sasa takwimu zinaonesha idadi ya wagonjwa inaongezeka kwa kasi Tanzania.

"[Walk the Talk] ni moja ya jambo ambalo tunalifanya kuhakikisha tunawekeza zaidi kwenye kinga badala ya tiba," amesema na kuongeza,

".., tunaona wagonjwa wengi wenye kisukari na magonjwa yasiyoambukiza, tunataka kuwekeza kwenye afya zetu kila mmoja achukue hatua.
Amesisitiza "Mimi ni mwanafunzi wa Prof. Janabi [Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili [MNH].

"Mmeniona nimepungua na niseme nitaendelea kupungua zaidi, [kimsingi] tule ila tusiendekeze tabia bwete [tufanye mazoezi ya kushughulisha mwili]," amesema.

Ameongeza "Serikali itaendelea kushirikiana na wadau mbalimbali kuhakikisha tunaendelea kuhimiza Watanzania kufanya mazoezi na kuzingatia mtindo bora wa maisha.

"Wiki ijayo nitashiriki MEWATA, tutatembea kuunga mkono mapambano dhidi ya saratani za wanawake.

"Kwa sababu wanataka pia kujenga Women Wellness Center [WWC] sehemu ambayo wanawake wataweza kwenda kujua afya zao, kufanya mazoezi ya pamoja kupata huduma za ushauri na tiba za kisaikolojia.

Amebainisha "Wikiendi nyingine nitatembea na LUKIZA Autism [April 28, 2024] ... kwa hiyo mimi watanzania kama kuna mtu anataka kutembea na waziri wa afya nipo tayari.

"Tutembee iwe sehemu ya kuhamasisha kujilinda na kujikinga na magonjwa yasiyoambukiza.,".

Awali amesisitiza mambo mengine ya msingi ambayo Serikali itaendelea kuyazingatia katika sekta ya afya ili kuiimarisha zaidi, Tanzania.

Ameongeza "Tutaendelea kuwekeza kwenye miundombinu ya watoa huduma za afya ikiwamo kujenga zahanati, vituo vya afya na hospitali kwa ngazi zote.

"Serikali itaendelea kuchukua hatua za makusudi ili kuendelea kuhakikisha afya kwa kila Mtanzania.

"Tutaendelea kuwekeza kuimarisha upatikanaji wa huduma za uchunguzi ikiwamo huduma za maabara na radiolojia.

"Tutaendelea kuwekeza katika kuimarisha upatikanaji wa rasilimali watu ya afya kwa ngazi zote kuanzia huduma za msingi hadi ubobezi.

"Tutaendelea kuimarisha upatikanaji wa dawa na elimu ya afya kwa umma," amesisitiza Waziri Ummy.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement