Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Ndoa 14,600 zipo ‘ICU’ migogoro tele imerekodiwa na bado haijapata ahueni/suluhu, 'ICU' ni chumba cha wagonjwa wahututi ambako mgonjwa huhitaji uangalizi wa karibu ili kunusuru uhai wake.

Idadi hiyo imerekodiwa kipindi cha Julai, 2023 hadi April, 2024 [yaani miezi 10] ofisi za Ustawi wa Jamii.

Migororo/mifarakano hiyo imerekodiwa pia ofisi nyinginezo ambazo zipo chini ya Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake, Watoto na Makundi Maalum.

Waziri Dkt. Dorothy Gwajima amebainisha hayo alipozungumza na waandishi wa habari punde baada ya kufungua Mkutano Mkuu wa 21 wa Mwaka wa Chama cha Madaktari Wanawake Tanzania [MEWATA].

“.., na hizo ndizo  zilizoripotiwa,” amesema na kusisitiza kwamba mifarakano, migongano na migogoro imekuwa ikichangia visa vingi vya kikatili vinavyoshuhudiwa ndani ya jamii.

Ameongeza “Mwisho wa siku tunaona ndoa imepasuka, lakini chembechembe gani za afya ‘determinats’ za afya [vizingatio] vya afya vipo mule?.

“Ukirudi huku tunaona kuna ujeuri, kutokuwa na heshima … kuna vitu vipo mule nani anavifanyia utafiti, [yaani]  tuzuie nini [au] tufanyeje tuzui?.

“Hii ni nguvu ya MEWATA kuingia kwa jamii, kuleta ule utengemao,” amesema Waziri Dkt. Gwajima.

Kwa mantiki hiyo amekialika rasmi Chama hicho kilichosheheni madaktari mabingwa na wabobezi katika nyanja mbalimbali za afya ili kushirikiana na Wizara hiyo bega kwa bega kwenda kuisaidia jamii.

Amesema amefungua milango wazi kwa MEWATA kwani wana nafasi kubwa na jamii inawaamini hivyo ni wakati mwafaka kwenda kuipatia maarifa yatakayoikomboa.

Makamu wa Rais wa MEWATA na Mtaalamu wa Masuala ya Afya ya Jamii Dkt. Mary Sando amesema wapo tayari kushirikiana na Serikali kupitia Wizara hiyo kuihudumia jamii.

“Sisi kama wanawake tunaotamani kuona afya ya jamii [inaimarika] na ukatili unatokomea tumefurahi kuwa naye [Waziri Gwajima] akimsaidia Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema.

Ameongeza “Kama mnavyofahamu sisi MEWATA huko nyuma tulikuwa tunaitwa ‘wapiga debe’ [yaani watu wanaovalia njuga suala fulani kwa maslahi mapana ya kuijenga afya ya jamii].

“Wote tunafahamu na tunaona ukatili wa kijinsia unavyoendelea, tunaamini tukiweza kwa utaalamu wa kisayansi [tuliojaliwa tutashirikiana na Wizara inayotengeneza miongozo.

“Tutaweza kusaidia kupiga hatua ambayo Wizara pamoja na wadau mbalimbali wanajaribu kufanya ili kutengeneza jamii iliyo na ustawi mwema,”.

Amesema Dkt. Mary ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji Mkuu wa Shirika la AAPH.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement