moja

Responsive Advertisement



Juni 19 kila mwaka ni Siku ya Siko Seli Duniani ilipitishwa na Umoja wa Mataifa [UN] mahususi kabisa kwa ajili ya jamii, kujengewa uelewa juu ya ugonjwa juu, pia kila nchi kuhakikisha ina Sera nzuri na miongozo ya kinga na tiba kwa raia yake, lengo hasa ni kuuvunja mduara wa Siko Seli. Mwaka huu kauli mbiu inasema 'Vunja Mduara, Pima Jua Hali yako ya Siko Seli' Shairi hili ni maalum limeandikwa na Veronica Mrema kwa ajili yako, karibu.
.
Kalamu nimeishika, Ninalo la kuwaambia,

Moyo nimeufungua, Tayari kuwaandikia.


Karibuni mjongee, Wake na waume pia,

Wasichana na Vijana, My wenu nawaeleza.


Ugonjwa Siko Seli, Bado wengi hamjui,

Si laana ya vizazi, Wala ndumba za wachawi.


Ni ugonjwa wa kurithi, Kwa vinasaba vya wazazi,

Wote baba na mama, Mtoto wanapomtengeneza.


Mimba inapoingia, baba na mama humpa,

Kinasaba cha ugonjwa, Kiumbe tarajiwa.


Si ugonjwa wa kuambukiza, Daima hili kumbuka,

Usimtenge mgonjwa, Usimfanyie unyanyapaa.


Tanzania inapambana, Kizazi chake kukomboa,

11,000 kila mwaka, Huzaliwa na ugonjwa.


Ni kati ya mataifa, yenye wengi wagonjwa,

Barani Afrika, Dunia nayo inajua.


Siko Seli huchangia, Vifo vingi vya watoto,

Chini ya 5 miaka, Kila mwaka Tanzania.


Uhai wakijaliwa, Maumivu ni makali,

Huyaishi daima, Kila siku ya maisha.


Damu kwisha mwilini, Na mateso mengi pia,

Hupitia kila mara, Kuugua na kulazwa.


Kuuvunja mduara, Vijana tuna dhamana,

Kabla ya kuanza ndoa, Watoto kuwaleta.


Muhimu chunguza afya, Hali yako ya kinasaba,

Umerithi ama la, Amua kwa busara.


Ikiwa una kinasaba, Chagua asiye nacho,

Hii ndiyo njia bora, Kuuvunja mduara.


Hapa natamatika, Ujumbe nimeufikisha,

Sina shaka umeelewa, Hatua chukua sasa.


Veronica Mrema 

M24 TANZANIA MEDIA

VRM19062024

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement