moja

Responsive Advertisement


Na Veronica Mrema

Sampuli ya bangi aina ya skanka imepelekwa maabara ili kuchunguzwa kwa kina zaidi kujua haswa ndani yake kuna kemikali gani nyinginezo zinazochanganywa na je athari zake ni zipi?.

Ni bangi ambayo ripoti za awali zinaeleza ina kiwango kikubwa mno cha kemikali yenye sumu aina ya Tetrahyrocannainol [THC] ambayo huharibu mfumo wa fahamu na akili ya binadamu.

THC inatajwa pia kusababisha magonjwa yasiyoambukiza [NCD’S] kama ya moyo na figo.

Wajawazito wanapotumia huenda kuathiri kiumbe kilichopo tumboni ikiwamo kuvuruga kabisa maendeleo ya ubongo wa mtoto.

Kemikali hiyo huweza kusababisha pia mtoto kuzaliwa na uzito pungufu, kabla ya wakati wake kutimia.

Wakemia wa Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya [DCEA] wanashirikiana kwa ukaribu na wenzao wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali [GCLA] kuichunguza Skanka.

Tanzania imeamua kufanyia uchunguzi zaidi kwa bangi hiyo baada ya kumtia nguvuni mhalifu kinara wa usafirishaji na uingizaji wa bangi hiyo nchini akiwa na kiasi cha kilogramu 1,815.

Hiyo ni sawa na shehena ya tani 1.8, zilizokamatwa katika oparesheni iliyofanyika Agosti 28, 2024 hadi Septemba 2, 2024 huko Luguruni Mbezi na Magomeni Jijini Dar es Salaam.

Jumla ya watuhumiwa watano tayari wamekamatwa kwa dawa hizo, Kamishna Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo amebainisha hayo katika mkutano wake na waandishi wa habari.

 “Wametueleza huko wanakozitoa, kuna maeneo wanakozisindika,” amesema na kuongeza ..,

“Wanazitoa nchi nyingine wanazileta nchi zingine wanasindika halafu zinafungashwa, zinaletwa hapa nchini.

“Baada ya kuwakamata tumeshawasiliana na hizo nchi husika, katika hayo maeneo ambayo wanashirikiana nayo katika kuleta dawa za kulevya nchini,” amesema.

Amesema kwa kuwa bado wanawatafuta hao wahalifu wengine wanashirikiana kwa ukaribu na nchi zilizotajwa na wahalifu hao hivyo hawatazitaja hadharani hivi sasa.

“Kwa sababu kulingana na taarifa tulizopata, zinatengenezwa kwengine, zinaletwa nchi nyingine kama bangi ambako kuna viwanda vidogo vodogo zinatengenezwa hizo skanka.

“Ndiyo maana tunafanya uchunguzi wa kimaabara, kule inakozalishwa oparesheni zinaendelea, ili kubaini pia hizo viwanda,” amesema.

Amewataja waliokamatwa “Ni Richard Henry Mwanri [47] mfanyabiashara na mkazi wa Mbezi Makonde, Wilaya ya Kinondoni Dar es Salaam.

“Felister Henry Mwanri [70] mkazi wa Luguruni Mbezi pia ni mmiliki wa nyumba zilipokutwa dawa hizo za kulevya.

“Watuhumiwa wengine ni Athumani Koja Mohamed [58] mfanyabiashara na mkazi wa Tanga, Omary Chande Mohamed [32] dereva bajaji na mkazi wa Buza Dar es Salaam.

“Juma Abdallah Chapa [36] mkazi wa Kiwalani Dar es Salaam [zimekamatwa pia] gari aina ya Mitshubishi Pajero yenye namba T 551 CAB na bajaji yenye namba MC 844 CZV.

 Aina hiyo ya bangi inayoshika kasi biashara na matumizi yake haitengenezwi nchini Tanzania.

Upo mnyororo mkubwa wa biashara hiyo ukihusisha mataifa mbalimbali ambako huzalishwa, huchakatwa na kisha kusafirishwa kuletwa Tanzania.

Amesisitiza Kamishna Jenerali Lyimo “Haitengenezwi Tanzania, zinatengenezwa nje baadae zinasafirishwa kimagendo, kwa njia za panya kuingiza nchini.

“Ndiyo [maana] tunataka sasa tuone, kwenye ule mchanganyiko labda kama kuna kemikali nyingine wanazoweka ili kuleta athari hasa katika mfumo wa fahamu.

“Baada ya kusindikizwa inakuwa na kiwango kikubwa cha THC, Mamlaka ina ‘divisheni’ ya sayansi jinai, ambayo inashughulika na masuala ya kimaabara ni wakemia.

“Ili kujua viwango, athari pia na kemikali ambazo zinakuwa kwenye dawa mbalimbali za kulevya ambazo tunazikamata wanachunguza.

“[Hivyo] matokeo yatakapopatikana, tutajulisha Umma kuhusiana na hilo suala,” amesisitiza.

Ameongeza “Viwango halisi vya hizi skanka ambazo zinawekwa na hawa wafanyabiashara.

“Kwa sababu hivi viwango vya kemikali wanavyoweka ni kwa ajili ya kufanya watu wawe waraibu lakini pia wawe wategemezi yaani unavyotumia uwe na hamu na usiweze kuacha.

“Sheria yetu hadi sasa hairuhusu uzalishaji wala usambazaji wa bangi hata nchi zilizoruhusu nazo zimejiwekea masharti si kwamba ikilimwa isambazwe mtaani kuna masharti yake.

Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa UNDC kuhusu hali ya dawa za kulevya duniani inaonesha jinsi baadhi ya maeneo ambako zimeruhusu matumizi ya bangi, hali haipo shwari hivi sasa.

“Kiwango cha matumizi kimeongezeka duniani, walikoruhusu kulima matatizo ya akili na watu kujaribu kujiua, imeongezeka katika maeneo hayo.

Ameongeza “Taarifa za matumizi ya dawa za kulevya zinaonesha pia uhalifu umeongezeka katika maeneo hayo.

“Pengine faida ya kuruhusu haya mambo inaweza ikawa ni ndogo kuliko hasara, kwamba hasara ni kubwa kuliko faida.

“Unaweza ukapata fedha lakini ile fedha ukaitumia katika kudhibiti uhalifu zaidi, unajikuta unatoa hapa unaweka hapa.

“Ndiyo maana sisi Tanzania Serikali haijaruhusu kilimo, wala biashara wala matumizi ya dawa za kulevya hapa nchini.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement