NA VERONICA ROMWALD – DAR ES SALAAM
TEKNOLOJIA inazidi kukua kadri miaka inavyosonga mbele. Wataalamu wa sayansi nao wanazidi kubuni vitu mbalimbali kwa ajili ya kusaidia kurahisisha maisha.
Kila siku vitu vipya vimezidi kuvumbuliwa katika ulimwengu huu, katika sekta tofauti tofauti ikiwamo sekta ya afya.
Pacemaker au maarufu nchini kama betri ya moyo ni miongoni mwa vifaa ambavyo vimebuniwa katika ulimwengu huu.
ambaye moyo wake unashindwa kuzalisha umeme wa kusukuma damu kwenda
kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
Mkurugenzi wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi.
Inaelezwa kwamba kwa mara ya kwanza kilianza kuwekwa katika mwili wa binadamu mnamo mwaka 1960.
Lengo la kuwekwa kwa kifaa hicho katika moyo wa binadamu ni kuwezesha kuzalishwa kwa umeme ili kusaidia kusukuma damu katika moyo unaoshindwa kusukuma kwa kutumia umeme wa asili.
Julai 15, mwaka huu Taasisi ya Tiba ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI) ilifanikisha kufanya upasuaji wa kupandikiza kifaa hicho katika moyo wa mtoto Happiness Josephat (6).
Kwamba moyo wake ulikuwa hauzalishi umeme wa asili kuwezesha misuli yake kusukuma damu kwenda kwenye sehemu nyingine za mwili wake.
Happiness alizaliwa Desemba 16, mwaka 2010 huko wilayani Mbulu mkoani Manyara. Alikuwa akipoteza fahamu kila siku mara nne hadi sita.
aliruhusiwa kurejea nyumbani, hata hivyo hali yake ilibadilika ghafla siku kadhaa kabla ya kurudi kliniki kwa uchunguzi zaidi katika Taasisi hiyo.
Kwanini watoto huzaliwa na tatizo hilo.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo kwa Watoto, Godwin Sharau anasema watoto 20000 huzaliwa na tatizo kama lile la marehemu Happiness kila mwaka.
Anasema watoto wengi hupata ugonjwa huu hutokana na ile nguvu ya kupiga maradhi ya mama ‘auto immune’ pale inapovuka katika kondo la mtoto wakati akiwa tumboni.
"Mtoto anakuwa ametungwa na moyo mzuri lakini zile nguvu za mama (antibody) zinavuka na kuingia kwenye damu ya mtoto na kusababisha huaribifu ‘heart brock’, " anasema.
Anasema iwapo itatokea hali hiyo ya antibodies kuvuka katika kondo la uzazi na kumfikia mtoto husababisha karibu asilimia 70 ya watoto hawa kufia tumboni.
Madaktari wakifanya upasuaji
"Hii ni kwa sababu ule uwezo wa moyo kusukuma damu mbele si mzuri, wanaopona ndiyo huwa kama marehemu Happiness kwetu JKCI ilikuwa jambo la ajabu kumpata mtoto yule.
"Watoto wengi hupoteza maisha kabla ya kufika hospitalini , kwa watu wazima inatokea sana na wengi huwekewa vifaa hivi, " anasema.
kupandikiza betri wagonjwa 31.
Daktari huyo (katikati juu) anasema Pacemaker, ni kifaa maalumu ambacho huwekewa mtu ambaye moyo wake unashindwa kuzalisha umeme wa kusukuma damu kwenda kwenye sehemu mbalimbali za mwili.
Anasema ni vifaa vinavyowekwa mwili tangu 1960 kwenye mwili wa binadamu, watu wasiopungua milioni 3, kila mwaka watu wapatao 600,000 huwekewa kifaa hicho.
Anasema hadi sasa watu wapatao milioni tatu tayari wamekwisha wekewa kifaa hicho duniani.
“Alipofika uwanja wa ndege alijisikia vibaya walipompima iligundulika kuwa mapigo yake hayafanyi kazi vizuri hivyo alifanyiwa upasuaji na kuwekewa kifaa hicho,” anasema.
Anasema wagunduzi wa kifaa hicho wanaendelea kukiboresha kila wakati.
"Miongoni mwa vitu vinavyoboreshwa ni ule uwezo wa nguvu inayowekewa ndani ili iweze kudumu muda mrefu na bado wanaendelea kuboresha.
Ushuhuda wa mgonjwa
Kikwete (JKCI).
Anasema aligundulika kuwa na tatizo la moyo mnamo mwaka 2010 naada ya kufanyiwa vipimo hapa nchini.
“Nilipogundulika kuwa na tatizo hilo, nilikwenda nchini India kwa matibabu zaidim, kule nilifikia katika Hospitali ya St Jude, ambapo nililazwa kwa matibabu,” anasema.
Profesa Msananga anasema Februari 2011, aliambiwa kwamba alihitajika kuwekewa kifaa hicho cha pace maker kwani mapigo yake ya moyo hayakuwa yanakwenda kama inavyotakiwa.
Rais Dk. John Magufuli akifurahia jambo na Profesa Janabi
Masharti magumu
mwenendo wa afya yake.
“Baada ya kuwekewa pace maker nilishauriwa kuwa mwangalifu katika ulaji wangu, hivyo huwa napendelea kula vyakula vya kuchemsha, nikienda kwenye sherehe mbalimbali huwa najiepusha kula vyakula kama vile wali, pilau.
“Huwa napendelea kula mbogamboga za majani kwa wingi mfano ‘caul flower’ hii mboga inafanana na kabeji, nakula maharage, samaki wa kuchemsha, ndizi, sukuma wiki, na matembele, matunda kama vile tikiti maji, apple, machingwa, mananasi, papai, haya matunda hutegemeana na msimu ulipo,” anasema.
Anasema hata hivyo huwa anapendelea zaidi kubeba juisi aliyoitengeneza kutoka nyumbani kwake na kwamba huepuka zile zinazouzwa madukani.
Anasema jambo lingine analotakiwa kulizingatia ni matumizi ya dawa anazopaswa kuzitumia kila siku.
nimeendelea kufundisha kama kawaida,” anasema.
Aanguka ghafla
moja wakati alipomaliza kupandisha ngazi kuelekea darasani kufundisha.
“Siku hiyo nakumbuka nilikuwa nimepandisha ngazi haraka haraka, nilipata shork, nikaanguka, wanafunzi wangu walikuja na kunisaidia kuniinua pale chini, nikawaambia wasiogope kwani nikipumzika kidogo nitakuwa vizuri.
“Kweli waliniacha nikampuzika nikarejea katika hali yangu ya kawaida na nikaendelea kufundisha. Kila siku huwa natumia dakika 45 kufundisha, na wakati mwingine huwa zinazidi,” anasema.
Marufuku kuweka simu upande wa moyo
Anasema hili ni miongoni mwa masharti ambayo watu wanaofanyiwa upasuaji wa kuwekewa pace maker hutakiwa kulizingatia.
Rais Mstaafu, Dk. Jakaya Kikwete akimjulia hali mmoja wa watoto waliofanyiwa upasuaji.
Anasema kila siku hutakiwa kunywa maji kiasi cha lita moja na nusu, lakini kwa upande wa komputa hakuna tatizo hivyo huwa inakaa mbele yangu kama kawaida,” anasema.
Anasema pia haruhusiwi kubeba kitu chochote chenye uzito.
“Nashukuru Mungu hadi majirani zangu wanajua hali yangu niliyonayo, zamani hata mlango ukibamizwa nilikuwa napata shida lakini sasa nimezoea naona kawaida,” anasema.
Moyo hupaswa kupiga mara 70
Mkurugenzi wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi anasema kwa kawaida kwenye moyo kuna ‘system’ imekaa kama umeme na hiyo ndiyo inayosafirisha mawasiliano ili moyo uwee kupiga na kupumzika.
“Kwa kawaida tunachotegemea moyo lazima upige mara 70 kwa dakika na utoe damu mililita 70, hivyo 70 mara 70 ni 490 ambazo ni sawa na lita tano na hiyo ndiyo dmu yetu kwa kawaida.
“ule mfumo ukibadilika mapigo ya mtu hupiga chini ya kiwango hicho na ndipo hapo unakuta wengi huzimia na kushindwa kufanya shughuli zao za kila siku za kijamii na kiuchumi,” anasema.
Anasema wapo ambao hupoteza fahamu kati ya mara tano hadi sita kwa siku.
Gharama ya pacemaker ni kubwa.
gharama za usafiri, chakula na malazi.
“Ni ghali kuweka pace maker, sasa wagonjwa wetu baadhi yao walikuwa na bima ya afya, hapa JKCI tunaweka kwa Sh milioni 8.5 kwa wale wasiokuwa na bima hadi milioni 40.
"Hivyo nawasihi watu kukata bima kwani ni lazima vifaa hivi vinunuliwe na vinapatikana nje ya nchi kwa gharama kubwa,” anasema.
Idadi ya waliofanyiwa upasuaji
"JKCI tunaweka pia vyuma kwenye mishipa iliyoziba, mwaka huu pekee wagonjwa zaidi 45 tumeshawawekea na wanaendelea vizuri.
"Tayari tumefanya upasuaji mkubwa wa kutibu moyo kwa kufungua kifua kwa watu 326.
"Upasuaji unafaywa kwa uangalifu mkubwa hadi sasa vifo vilivyotokea ni vinane tu, " anasema.
Moyo ni nini
Kikundi cha Baps Charity kikikabidhi msaada wa fedha kusaidia matibabu ya watoto kwenye taasisi hiyo, hivi karibuni
Kwa kawaida moyo wa viumbe walio katika kundi la mamalia ikiwa ni pamoja na binadamu huwa una pande mbili.
Upande wa kulia huwa unasukuma damu kwenda mapafu inapopokea oksijeni, upande wa kushoto unazungusha damu katika sehemu nyingine za mwili pale ambako oksijeni iliyopokelewa huhitajika.
Inaelezwa kwamba moyo ni ogani ya lazima kwa uhai. Mishipa ya damu moyoni huwa na majina maalumu.
Kwa jumla kuna mishipa mikubwa kwa sababu damu yote inapaswa kupita humo.
Kwa hiyo mishipa karibu na moyo ni kama barabara kuu za damu mwilini.
Mishipa yote inayopeleka damu kwenda moyoni huitwa vena.
Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ummy Mwalimu akiwa na Mkurugenzi wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi hivi karibuni alipotembelea taasisi hiyo.
Ateri kuu inayopeleka damu mwilini inaitwa aorta. Zipo pia ateri za nje zinazozunguka moyo mwenyewe.
Chapisha Maoni