Jumla ya kinamama wajawazito 35 wamefamyiwa uchunguzi wa kipimo cha magonjwa ya moyo kwa
watoto wachanga waliopo tumboni mwa mama zao (FETAL ECHOCARDIOGRAPHY) ili
kujuwa kama wanamatatizo ya moyo au la.
Majibu
ya kipimo hicho yalionyesha kuwa kati ya hao watoto watano walikutwa na
matatizo ya moyo jambo ambalo litawawezesha kupata
matibabu mapema pindi watakapozaliwa.
Hayo
yamesemwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya
Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani wakati akiongea na waandishi wa habari
hivi karibuni.
Dkt.
Naiz alisema kipimo hicho hakina madhara yoyote kwa mama na mtoto na kina uwezo wa kugundua endapo mtoto ameathirika na
ugonjwa wa moyo na hivyo kumuandaa mama mjamzito kwaajili ya uzazi salama.
“Mojawapo
ya dalili za mama mjamzito ambazo zinaweza pelekea kupata mtoto mwenye tatizo la ugonjwa wa moyo ni pamoja na
ugonjwa wa kisukari,shinikizo la damu,matumizi ya dawa za muda mrefu,mimba ya
mapacha, kuwepo na mtu mwenye tatizo la moyo katika familia na mimba pandikizi”.
“Ninawaomba
kina mama wajawazito wenye moja ya dalili nilizozitaja waje tuwafanyie
kipimo hiki
kipindi ambacho mimba zao zitakuwa na umri wa kati ya
miezi minne hadi saba hii itawasaidia kugundua afya za watoto wao na
kuepuka na vifo vya mara baada ya kuzaliwa vinavyotokea kipindi cha
mwezi mmoja hadi mwaka”, alisema Dkt.
Naiz.
Alizitaja
changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na uelewa mdogo wa kinamama wajawazito
juu ya kipimo hicho kwa kufikiria kuwa kinamadhara jambo ambalo siyo kweli kwani kipimo hicho
hakina madhara yoyote kiafya.
Taasisi
ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) ilianza
kutoa huduma hiyo tangu mwezi wa tatu mwaka huu ili kupunguza vifo vya
watoto vinavyotokana na magonjwa ya moyo mara baada ya mtoto kuzaliwa.
Chapisha Maoni