Picha na mtandao
Na Veronica Romwald, Dar es Salaam
Mwanaume anayeshiriki vema tendo la ndoa kwa
kiwango kinachostahili hujiepusha kupata saratani ya tezidume kuliko yule
ambaye hufanya kwa kiwango kisichostahili.
Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Saratani wa Taasisi
ya Ocean Road, Mark Mseti alisema hayo alipozungumza na MTANZANIA katika
mahojiano maalumu.
Alisema zipo tafiti ndogondogo ambazo zimewahi
kufanyika duniani zinazothibitisha ukweli juu ya jambo hilo.
“Hazijawahi kufanyika tafiti kubwa, lakini
inaelezwa angalau mwanume aliyekamilika anapaswa kushiriki angalau mara tatu
kwa wiki ingawa wapo pia ambao hujiweza na kuvuka zaidi ya hapo,” alisema.
Aliongeza “Hii haimaanishi kuwa mzinzi… ukiwa
mzinzi maana yake utapata magonjwa mbalimbali hasa ya zinaa na hivyo kujiweka
kwenye hatari zaidi.
Hapa nimekuwekea kwa kifupi, habari hii imetoka leo kwa kina kwenye gazeti la MTANZANIA, hivi karibuni usikose nakala yako alhamis ambapo utasoma kwa undani makala ya mahojiano na Dk, Mseti ameeleza kwa kina kuhusu tatizo hilo, visababishi vingine, dalili na matibabu yake.
Chapisha Maoni