Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Profesa Mohamed Janabi, (wa pili kushoto), Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Peter Kissenge na Meneja wa Kanda wa Kampuni ya Samiro Pharmacetical, Masila Mani.g wakiwa katika picha ya pamoja na Mfanyakazi bora wa mwaka 2017 JKCI, Muuguzi Mkuu Mwandamizi wa JKCI, Hadija Mnadi.

Na Mwandishi Maalum, Dar es Salaam

Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI), Profesa Mohamed Janabi amewatunuku vyeti na zawadi wafanyakazi bora wa mwaka 2017.

Hafla hiyo imefanyika mapema leo katika ukumbi wa mikutano wa Taasisi hiyo, vyeti na zawadi hizo zimetolewa na Kampuni ya Samiro Pharmacetical.

Akizungumza, Prof. Janabi amesema hatua hiyo imelenga kuwapa motisha wafanyakazi wake ili wazidi kufanya kazi vyema zaidi katika kuhudumia wagonjwa wanaowapokea.

“Taasisi yetu inafanya uchunguzi na kutoa matibabu kwa watu ambao wanakabiliwa na magonjwa ya moyo, tunatoa huduma bora na ndiyo maana tunaona tuwape motisha wafanyakazi wetu ili wazidi kufanya kazi kwa bidii na tuzidi kutoa huduma bora zaidi,” amesema.

Aliwataja wafanyakazi waliotunukiwa vyeti na zawadi ni Daktari Bingwa wa Watoto, Stella Mongella, Ofisa Mtunza Kumbukumbu za Utabibu (THR II), Maimuna Hemed, Daaktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Aloyce Mohamed na Nesi Mkuu Mwandamizi Hadija Mradi.

Sambamba na hilo, Profesa Janabi amesema wamepanga kuanza kuwakopesha wafanyakazi wake mikopo mbalimbali.

“Tunataka tuwakopeshe wenyewe humu ndani kwa sababu kwenye taasisi zingine unakuta wanaweka riba kubwa, tukiwakopesha itawasaidia mno kiuchumi,” amesema.


Naye, Meneja wa Kanda wa Kampuni ya Samiro Pharmacetical, Masila Mani.g amesema kampuni yao imekuwa na utaratibu wa kuwezesha vyeti na zawadi hizo kwa muda mrefu sasa katika taasisi hiyo.

“Si mara yetu ya kwanza, tunafanya hivi kwa sababu tunawajibika pia kurejesha kwa jamii na hatua hii inasaidia kuwapa motisha wafanyakazi hawa ili wazidi kutoa huduma bora kwa jamii,” amesema.
Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Prof. Janabi akimtunuku cheti Daktari Bingwa wa Watoto, Stella Mongella wakati wa hafla hiyo.

Mkurugenzi Mtendaji wa JKCI, Prof. Janabi akiwa katika picha ya pamoja na Daktari Bingwa wa Watoto, Stella Mongella na Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Peter Kissenge na Meneja wa Kanda wa Kampuni ya Samiro Pharmacetical, Masila Mani.g.
Mkurugenzi wa JKCI, Prof. Janabi akimtunuku cheti na zawadi, Ofisa Mtunza Kumbukumbu za Utabibu (THR II), Maimuna Hemed.

Mkurugenzi wa JKCI, Prof. Janabi akimtunuku, Daktari Bingwa wa Magonjwa ya Moyo, Aloyce Mohamed wakati wa hafla hiyo.

Mkurugenzi wa JKCI, Prof. Janabi akizungumza na wafanyakazi wakati wa hafla hiyo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement