SUALA la upungufu wa nguvu za kiume hivi sasa ni gumzo si hapa nchini pekee, bali dunia nzima, kulingana na utafiti mpya uliofanyika huko nchini.
Utafiti mpya uliofanywa kwa wanaume 5,177 umebaini wanaume
wenye mbegu chache za kiume wana mafuta mengi mwilini, shinikizo la damu na
mafuta machafu katika mishipa ya damu.
Matokeo ya utafiti huo yanaeleza wanaume wenye mbegu chache
za kiume wako katika hatari ya kupata magonjwa kulingana na utafiti mpya.
Yanaeleza wanaume hao pia wana uwezo mkubwa wa viwango
vidogo vya homoni za kiume. Waanzilishi wa utafiti huo wamesema wanaume wenye
mbegu chache za kiume pia ni muhimu kufanyiwa vipimo vyengine vya magonjwa
mengine.
Hivi karibuni nchini Tanzania kumeshamiri kwa uwepo wa
matangazo mbalimbali ambayo mengine ni rasmi na mengine sio rasmi kuhusiana na
dawa za asili haswa za kuongeza nguvu za kiume lakini sasa serikali ya nchi
hiyo imethibitisha matumizi ya dawa tano za asili.
Huku miongoni mwa dawa hizo ni dawa ya 'Ujana' ambayo kazi
yake ni kusaidia kuongeza nguvu za kiume wakati dawa nyingine zikiwa Sudhi,
Vatari, IH Moon na Coloidal Silver ambazo kazi yake ni kukemea vimelea
mbalimbali.
Baraza la dawa nchini humo limesema hatua hii imekuja baada
ya uchunguzi wa kina uliofanywa na kubaini kuwa dawa hizo hazina madhara kwa
afya ya binadamu hivyo hawana budi kuzikubali.
Aidha Paul Muhame ambaye ni Kaimu Mkurugenzi wa dawa za
asili nchini Tanzania anasema baada ya baraza kupitisha vigezo vyote vilivyohitajika
kutoka katika dawa hizo na mamlaka ya dawa na chakula wamethibitisha hilo.
"Suala la muhimu ambalo tumeliangalia zaidi ni usalama
wa mtumiaji lakini katika upande wa kuthibitisha kuwa dawa hizo zinaponyesha au
la, linabaki kwa mnunuaji na mtumiaji wa dawa hiyo''.
'Hatari'
Upungufu wa mbegu za kiume na matatizo ya ubora wa mbegu
hizo ni maswala yanayoathiri mmoja kati ya wanandoa watatu kushika mimba
kulingana na utafiti huo uliofanywa nchini Uingereza.
Lakini katika utafiti huu mpya wanasayansi walichanganua
wanandoa wasioweza kupata watoto nchini Itali kujua iwapo ubora wa mbegu hizo
pia unaathiri afya ya mtu kwa jumla.
Waligundua kwamba wanaume wengi walio na mbegu chache
walikuwa na matatizo kadhaa ya kiafya ikiwemo mwili ulionenepa na shinikizo la
damu.
Hatua hiyo huongeza hatari ya kupata ugonjwa wa kisukari,
magonjwa ya moyo na kiharusi.
Wanaume hao pia walionekana kuwa na viwango vya juu vya
kuwa na homoni chache za kiume ambazo hupunguza ukubwa wa misuli na mifupa na
huenda vikasababisha ugonjwa wa kudhoofika kwa mifupa.
Daktari Albert Ferlin ambaye aliongoza utafiti huo ,
alisema: Wanaume wasio na rutuba hukumbwa na matatizo ya kiafya ambayo yanaweza
kuhatarisha hali yao ya maisha na kupunguza kiwango cha maisha wanayoishi.
''Rutuba huwapatia wanaume fursa isio ya kawaida ya kutathmini afya na kuzuia
magonjwa''.
Haki miliki ya picha Getty Images Image caption Watafiti
wanasema kuwa ubora wa mbegu za kiume unaathiri afya ya wanaume.
Hata hivyo wamiliki wa utafiti huo walisisitiza kuwa
utafiti wao haukuthibitisha kuwa ukosefu wa mbegu za kiume za kutosha
husababisha matatizo ya kimetaboliki lakini badala yake ni vitu viwili
vinavyohusiana.
Wanasema kuwa uhaba wa homini za kiume uhusishwa na
matatizo haya ya kiafya.
Dr. Ferlin alisema kuwa utafiti unaonyesha kwamba ni muhimu
kwa wanaume wanaotibiwa matatizo ya ukosefu wa rutuba wanafaa kuangaziwa vizuri
kimatibabu.
''Wanaume walio na matatizo ya kuwapatia mimba wake zao
wanafaa kukaguliwa vizuri na kufuatiliwa na wataalam wao wa rutuba kwa sababu
huenda wana viwango vya juu vya kupata maradhi na vifo'', alisema.
Chanzo
BBC
Chapisha Maoni