Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement




Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam


wanafunzi wakifanya mtihani.

OFISI ya Waziri Mkuu Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) imesema Juni, mwaka huu itatangaza majina ya wanafunzi wanaotarajia kujiunga na masomo ya Kidato cha tano


Katibu Mkuu wa TAMISEMI alisema hayo hivi karibuni alipozungumza na MATUKIO NA MAISHA jijini Dar es Salaam lilipotaka kujua ni lini watataja shule walizopangiwa wanafunzi hao na hatma ya shule za Serikali zilizofungwa kutokana na ukosefu wa chakula.


“Kwa kawaida wanafunzi waliofaulu kwenda kidato cha tano wanatakiwa kufika shule mwezi Julai… kwa hiyo TAMISEMI tunatarajia kuwatangazia mapema kabla ya Juni 15, mwaka huu, wajue shule wanazotakiwa kwenda weze kufika ili wakaanze masomo yao mara moja,” alisema.


Akizungumza juu ya hatma ya shule zilizofungwa hivi karibuni alisisitiza kwamba Serikali haitambui kufungwa kwa shule hizo na kwamba imewaagiza waajiri  kuchukua hatua.


“Kufunga shule ni suala la kitaifa na ili ifungwe lazima waajiri  wajue niliwaagiza wachukue hatua kwa wale waliofunga shule hizo,” alisema


April 13, mwaka huu akizungumza na waandishi wa habari jijini hapa Sagini alisema fedha hizo za chakula hutolewa kwa awamu na kukamilishwa katika kipindi cha mwaka wa fedha unaotekelezwa.


Alisema Serikali hutoa huduma ya chakula kwa shule za sekondari za bweni na shule za msingi elimu maalum za bweni kwa kuzingatia fedha zilizotengwa na upatikanaji wake katika mwaka husika.


Alisema kati ya Julai 2014 hadi Machi 2015, Serikali ilitoa Sh bilioni 28.1 kwa ajili ya chakula cha wanafunzi ambazo ni sawa na asilimia 66.7 ya Sh bilioni 42.1 zilizotengwa kwa mwaka 2014/15. Kiasi kilichobaki ni Sh bilioni 13.9 sawa na asilimia 33.23 ya fedha zilizotengwa,”alisema.


Baadhi ya shule ambazo zilifungwa ni Rugambwa, Kahororo, Nyakato, Ihunga (Kagera), Lyamungo (Kilimanjaro), Mpwapwa, Abeid Aman Karume (Dodoma), Kazima, Milambo, Tabora wasichana na wavulana

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement