Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
Jengo la Moyo la Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Dar es Salaam

IDARA ya Tiba na Upasuaji Moyo Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) kwa kushirikiana na Hospitali ya Prince Sultan Cardiac Center iliyoko Riyadhi nchini Saud Arabia, itatoa huduma ya upasuaji wa kuziba matundu yaliyoko kwenye moyo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Dk. Hussein Kidanto alisema upasuaji huo utafanyika pasipo kufungua kifua kama ilivyozoeleka.

Alisema MNH imeanza kutoa huduma hiyo tangu jana hadi May 16, mwaka huu na kwamba wagonjwa zaidi ya 20 (watoto)wanatarajiwa kupatiwa matibabu.

Alisema tiba hiyo hufanyika kwa kutumia kifaa maalum cha kuziba sehemu yenye tundu kupitia mishipa ya moyo.

“Taaluma ya matibabu inabadilika kwa kasi kubwa duniani na ili tuweze kwenda sambamba na kasi hiyo ni lazima tushirikiane na nchi nyinginezo zilizopiga hatua kubwa kwenye nyanja mbalimbali za matibabu,” alisema.

Alisema MNH imepokea madaktari bingwa hao kupitia taasisi ya Al Mutanda Islami Trust ya nchini Uingereza.

“Wataalam wetu watajifunza ujuzi huo kutoka kwa wataalamu hao jambo ambalo litasaidia kupunguza kasi ya wagonjwa wanaoelekwa kutibiwa nje ya nchi katika siku za usoni.

kwa upande wake, Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo MNH, Dk Sulende Kubwoja alisema huduma hiyo itatolewa kwa watoto wenye umri sifuri hadi miaka 18.

Aliwataka watanzania kujitokeza kutoa damu ili iweze kutosheleza katika kipindi chote cha upasuaji huo.

Naye Daktari Mshauri na Mwelekezi wa Magonjwa ya Watoto wa Hospitali ya Prince Sultan, Profesa Jameel Alate alisema wameweza kutoa huduma kama hiyo kwa nchi ya Sudan na Yemen na kwamba lengo lao ni kuwasaidia watoto kupona tatizo hilo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement