Ndani ya hifadhi ya Eland Game Reserve iliyoko KwaZulu-Natal,
South Africa mwendesha baskeli alikatisha siku ya June 14 2015,
akakutana na chatu mkubwa mzima kabisa aliyeonekana kama amekula na
kushiba kupita kiasi… akampiga picha na kushare na watu wake mitandaoni.
Watu
wengi walisogea pia nao kujionea tu jinsi chatu huyo alivyo kwa sababu
sio kawaida unaweza kukutana na Chatu alafu akakuacha hivihivi… Siku
sita baadae yule chatu alikutwa amekufa, wakaja walinzi wa hifadhi hiyo
wakampasua ili kujua nini kilichomfanya afe !!
Kumbe chatu alikula nungunungu.. ndani ya
tumbo kakutwa nungunungu huyo japo hawana uhakika kama ni kweli
nungunungu kasababisha kifo cha chatu huyo.
Unaweza kujiuliza Chatu alianzaje kula Nungunungu na hiyo miba yote !!
Nungunungu alivyotolewa kwenye tumbo la Chatu
Miba ya Nungunungu iliyokutwa ndani ya tumbo la Chatu.
Chapisha Maoni