Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

MAISHA ya watu katika nchi zinazoendlea ikiwamo Tanzania yapo hatarini kutokana na asilimia 50 ya magonjwa yasiyoambukiza kusababisha vifo.

Aidha magonjwa hayo yamekuwa yakisababisha  ulemavu huku gharama za matibabu zikiwa kubwa hali inayopelekea tatizo hilo kuongezeka na kuwa kubwa zaidi katika nchi hizo.

Yalizungumzwa hayo mwishoni mwa wiki jana jijini Dar es Salaam na Kaimu Mkurugenzi Magonjwa yasiyoambukiza, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Dk. Auson Rwehimbiza katika semina na waandishi wa habari iliyolenga  kukamilisha mkakati pamoja na mpango kazi
 2015/2020.

Alitaja baadhi ya magonjwa hayo yasiyoambukiza ni moyo na mishipa ya damu, kisukari, kansa na magonjwa sugu ya mfumo wa hewa.

Alisema magonjwa hayo yanazidi kuongezeka nchini hasa kwa jamii ya watu waishio mjini na kuongeza kuwa watu wazima wenye umri wa miaka 80 kuwa na magonjwa hayo kwa asilimia moja hadi tatu na msukumo wa juu wa damu kwa
 Asilimia tano hadi 10.

"Tathmini ya mwaka 2012 iliyohusisha watu wazima katika wilaya 50, inaonesha viwango vya kisukari viliongezeka kwa asilimia tisa, huku asilimia 27 kwa msukumo wa juu wa damu," alisema Dk. Rwehimbiza.

Alisema ongezeko hilo limetokana na kuongezeka kwa utandawazi, ukuaji wa miji, kutofanya mazoezi ya mwili, ulaji usiofaa, utumiaji wa tumbaku pamoja na unywaji wa pombe
kupita kiasi.

Alisema Tanzania ilianza kujihususha na magonjwa yasiyokuambukiza kuanzia mwaka 2009 hadi 2015, kwa kuandaa mpango mkakati na mpango kazi ambao ulihusisha utekelezaji wa mpango wa taifa wa kisukari kwa kushirikiana na chama cha wagonjwa wa kisukari nchini.

 "Hadi sasa utekelezaji wa mpango wa taifa wa kuanzisha kliniki za magonjwa yasiyoambukiza umefikia asilimia 75 katika hospitali za mikoa na wilaya na vituo vya afya, asilimia 75 ya elimu zinazotolewa na watoa huduma wa afya katika hospitali za mikoa, wilaya na vituo vya Afya.

Aliongeza kwamba, Shirika la Afya Duniani (WHO), liliandaa mpango mkakati ambao ulidhamiria kupunguza viwango vya sasa vya vifo vitokanavyo na magonjwa hayo kwa asilimia 25 ifikapo mwaka 2025 na kupendekeza mapendekezo ya hiari lengo ikiwa kufanikiwa kwa mkakati huo.

Alisema hadi sasa wapo katika maandalizi ya kutoa elimu kwa jamii ya watu wa kansa,
umoja wa magojwa ya moyo, umoja wa magonjwa sugu ya mfumo wa hewa pamoja na chama cha wagonjwa wa kisukari nchini lengo ni kupunguza magonjwa hayo nchini.

Alisisitiza kwamba ulaji wa vyakula unaofaa na kufanya mazoezi ni moja ya njia za kuepukana na magonjwa hayo ambayo madhara yake yanapelekea ulemavu na vifo na kuongeza kuwa gahrama za matibabu kuwa kubwa .

Kwa upande wake Meneja Mradi John Garder alisema jamii kujenga taratibu za kupima afya
zao ili kujua afya zao mapema na kutafuta ufumbuzi endapo watakutwa na magonjwa kama hayo yasiyaombukiza na kuanza tiba mapema ikiwa ni pamoja na kupunguza gharama za matibabu,vifo na ulemavu.

Alilitaka, Shirika la Viwango Tanzania (TBS), kufanya uhakiki wa kushtukiza mara kwa mara wa bidhaa zilizopo madukani kwani bidhaa nyingi zimepita muda wa matumizi na kupelekea magonjwa.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement