Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement



 

 
OFISI ya Makamu wa Rais (OMR) imesema kusambaa kwa mifuko ya nailoni (plastick) pamoja na suala la  muungano ni mambo ambayo yaliipa changamoto kubwa katika kipindi cha miaka kumi ya uongozi wa Serikali ya awamu ya nne chini ya Rais JakayaKikwete.                                                                                     
Yalibainishwa hayo hivi karibuni jijini Dar es Salaam na Naibu Katibu Mkuu (OMR) Angelina Madette (pichani) alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu mafanikio na changajmoto walizokumbana nazo katika kipindi hicho.

“Katika kipindi cha awamu ya nne suala la muungano lilitupa changamoto na kuendelea kuwepo kwa mifuko ya plastiki isiyokidhi vigezo,” alisema.

Alisema katika kukabiliana na usambaaji wa mifuko hiyo OMR imekuwa ikiongea na watengenezaji ili watengeneze iliyokuwa na viwango vinavyohitajika.

“Lakini pia temeandaa kanuni ambazo zinaeleza kwamba lazima kiwango cha unene wa maikroni 50 pamoja na kuhamasisa matumamizi ya mifuko mingine kama mbadala,” alisema.

Hivi karibuni akijibu swali Bungeni mjini Dodoma,  Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais Mazingira Stephen Masele aliwataka watanzania kuacha kutumia mifuko hiyo katika kuhifadhi chakula kwani ina madhara.

Masele alikiri kuwa mifuko hiyo inaweza kusababisha madhara kutokana na kemikali zilizotumika kuitengeneza.

Alisema kemikali hiyo inapoingia katika chakula hugeuka kuwa sumu na kwamba serikali ilipiga marufuku matumizi ya mifuko hiyo yenye unene wa chini ya maikroni 30.

Katika changamoto ya muungano, Madette alisema kuliibuka hoja mbalimbali juu ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar ambapo waligundua kwamba elimu ya kutosha kwa wananchi inahitajika.

“Kuanzia 2006 hadi 2011 Hoja 15 za Muungano ziliwasilishwa na kujadiliwa na kamati ya pamoja iliyojumuisha nchi zote mbili,  kati ya hizo hoja kumi zimekamika na kuondolewa katika orodha ya changamoto na sita zinaendelea kutafutiwa ufumbuzi,” alisema.                                                 

Alisema hoja zilizopatiwa ufumbuzi katika kipindi hicho ni sheria ya Tume ya Haki za Binadamu kutofanya kazi Zanzibar kutokana na sheria hiyo kutokuwa ya muungano.

Alisema sheria nyingine ya uvuvi katika ukanda wa Bahari kuu, nafasi ya Zanzibar kuwasilishwa katika miradi ya maendeleo ya kiuchumi kwa ajili ya miradi ya kikanda inayotekelezwa na Jumuiya ya Afrika Mashariki.

“Miradi ya Zanzibar iliwasilishwa katika Jumuiya ambayo imefikia katika hatua mbalimbali ni mradi wa uwanja wa ndege wa Pemba, ujenzi wa bandari ya Maruhubi, ujenzi wa chelezo na kivuko cha kati ya bandari ya Zanzibar, Dar es Salaam, Pemba, Tanga na Mombasa pamoja na mgawanyo wa mapato yatokanayo na misaada kutoka nje ya nchi,” alisema.

Alisema changamoto nyingine ambazo zipo katika hatua ya kutafutiwa ufumbuzi ni ushirikiano wa Zanzibar na taasisi za kimataifa, utafutaji na uchimbaji wa mafuta na gesi asilia, taarifa ya mapendekezo ya Tume ya pamojaya fedha, kodi nyinginezo pamoja na usajili wa vyombo vya moto.



Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement