*Wamiliki
walia na ushuru mpya.
* Madereva walia na posho zao. wasema mgomo ni kuanzia wiki ijayo
CHAMA
cha Wamiliki wa Mabasi Tanzania (Taboa), kimesema mgomo wa mabasi nchini nzima unanukia, endapo Serikali
haitashusha gharama za ushuru wa kuingiza mabasi mapya.
Akizungumza
na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Katibu Mkuu wa Taboa, Ennea
Mrutu, alisema Serikali imewataka wamiliki wa mabasi kulipa asilimia 25 kama
ushuru kwa kila basi jipya linaloingizwa nchini.
“Zamani
tulikuwa tunalipa asilimia 10, sasa wamepandisha kiasi hiki, nani atamudu
gharama za uendeshaji?
“Basi
moja tulikuwa tunalipa Sh milioni 40, sasa tunatakiwa kulipa Sh milioni 94…
jamani gharama hizi ni kubwa, mbona tutashindwa kuhudumia Watanzania.
“Kwa
hali ya kawaida hatuwezi kukomboa basi, fedha hizi zitatoka wapi jamani? Tuwe
wakweli katika hili, kama utaratibu huu ukiendelea hatutaweza kusafirisha
abiria,” alisema Mrutu.
Alisema
wamiliki hao ambao walikuwa nchini China hivi karibuni, tayari wamekutana na
watengenezaji wa mabasi aina ya Yutong ambao wamekubali kuja Tanzania
kuzungumza na viongozi wa Serikali waone namna ya kuingiza mabasi mengi zaidi.
Mrutu
alisema kama Serikali ikiendelea na msimamo huo, ni wazi kuanzia sasa mgomo wa
kusitisha huduma hiyo unanukia.
“Kama
Serikali itaendelea na msimamo huu, tutasimamisha huduma, tumeleta mabasi mengi
yako bandarini, tumeshindwa kuyakomboa,” alisema Mrutu.
Alisema
bajeti kuu ya Serikali ya mwaka 201/16, haikuweka kipengele chochote cha
kupandisha gharama za ushuru, lakini wanashangazwa na hatua hii sasa.
Kutokana
na hali hiyo, Mrutu alisema Taboa imewaandikia barua Waziri wa Uchukuzi, Katibu
Mkuu Wizara ya Fedha, Waziri Mkuu na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA).
Akijibu
malalamiko hayo, Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, alikiri kupokea barua ya Taboa
na kusema Serikali inalifanyia kazi suala hilo mara moja.
“Nimepokea
barua yao, nashangaa kuona wamekuja kwa waandishi wa habari hata kabla
hatujazungumza, jambo kubwa ni kwamba tunashughulikia suala lao.
“Kwavile
wao wametoa tamko kwenu, na sisi tunajipanga kutoa taarifa rasmi. Nawaomba
wajue tulitoa punguzo kwa mradi wa mabasi ya mwendo kasi tu (DART),” alisema
Waziri Mkuya.
WAKATI HUO HUO
MADEREVA
nchini wametishia kufanya mgomo kwa mara nyingine kuanzia wiki ijayo na
kwa muda usiojulikana iwapo serikali kupitia kamati iliyoundwa
kushughulikia matatizo yao haitawaita na kuongea nao kuhusu posho zao za
ndani na safari za nje.
Kauli
hiyo imetolewa jijini dar es Salaam jana na Katibu mkuu wa Chama cha
Madereva, Rashid Salehe (pichani) ambapo alisema madereva hao wamemtuma na kuitaka
serikali isimuulize kiongozi yeyote wa madereva kipindi watakapoamua
kugoma mpaka madai hayo yatekelezwe.
Alisema
kuwa pamoja na kupata mikataba mipya katika kikao cha mwisho
kilichofanyika mwezi uliopita hata hivyo bado madereva wanaendelea
kupewa mikataba mingine tofauti na ile waliokubaliana katika kikao hicho
cha mwisho.
“Madereva
bado wanaendelea kupata shida na kusota bila kujua hatima ya posho zao
za safari za ndani na nje hivyo tunaitaka Wizara ya mambo ya Ndani na
Wizara ya Kazi isije kutuita viongozi na kutuuliza juu ya hili kwa kuwa
madereva hao wamechoka hivyo wamenituma baada ya kufanya ziara za mikoa
kadhaa na kuniagiza niseme kuwa wataacha kuendesha magari kama serikali
haitawaita kujua hatima ya suala hilo” alisema Salehe.
Aliongeza
migogoro kati ya madereva na matajiri wa magari hayo ni kutokana na
mfumo wa viongozi wa serikali kuhusika kuwafanya biashara hiyo huku
wakiwa wanawakandamiza waliochini.
“Kuna
kampuni ya magari fulani sitayataja jina tajiri wake analugha za matusi
na tumeshamrekodi wakati akitoa matusi hayo na tunafikiria kumpeleka
huyu bwana mahakamani” alisema Salehe.
Alisema
kuwa pia kuna gari la kigogo mmoja ambalo lilibeba sumu za mgodini
limekwama porini muda mrefu na tajiri wa basi hilo amewatelekeza
madereva hao bila kujali afya zao zinaendelea kuharibika kwa kukaa na
sumu hiyo.
Salehe
alisisitiza kama mfumo uliopo wa vigogo wa sarikali kuwa ndio wamiliki
wa mabasi hayo basi kila watakalo kuwa wanafanya litaonekana la kitoto
na migogoro haitaisha na ukizingatia wanalindwa na sheria ya mwaka 1955
ambayo wanaitumia mpaka leo.
Chapisha Maoni