Christy Sims ni
mwanadada ambaye maisha yake yalibadilika ghafla baada ya aliyekuwa
mpenzi wake wa muda mrefu kumuachia majeraha ambayo hatokuja kuyasahau
maishani.
Akiwa
na miaka 40 Christy amelazimika kuishi na makovu baada ya kumwagiwa
tindikali na ex-boyfriend wake kwa sababu tu ya wivu wa mapenzi.
Christy alikumbana na mkasa huo baada ya ex- boyfriend huyo kumhisi kuwa anatembea na mtu mwingine.
Christy Sims kabla ya tukio la kumwagiwa tindikali.
Haya
yote yalitokea weekend moja ya mwaka 2013 nyumbani kwa mpenzi wake
ambaye aliamua kumwagia dada huyu tindikali usoni,
kifuani na mikononi kitendo kilichosukumwa na hasira kali za wivu.
Christy alipiga
kelele nyingi na kuomba msaada lakini boyfriend wake aliamua kumuacha
aungue mpaka watu wa huduma ya kwanza walipofika na kushangazwa kwa nini
boyfriend huyo hakuchukua hatua za kumpatia girlfriend wake huduma ya
kwanza.
Christy Sims sasa hivi analazimika kuvaa miwani ya jua kila muda kulinda macho yake yasipigwe na jua la kumuumiza.
Jamaa
alijitetea na kusema ilikuwa ni bahati mbaya lakini Mahakama imeona
kuwa mwanaume huyo ana makosa 3, shambulio la kudhuru mwili, na makosa
mengine mawili ambayo kwa yote atatumikia kifungo miaka 60, miaka 20
kwa kila kosa
Chapisha Maoni