Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


Kidimbwi cha kuogelea chenye urefu wa mita 25 kinachounganisha kilele cha majumba mawili marefu yenye ghorofa 10 kitajengwa mjini London.
Kidimbwi hicho kinachoitwa ''Sky Pool'' ni cha kwanza duniani na kitakuwa na eneo la chini lililo wazi.Uwazi huo utawasaidia waogoleaji kuwaona raia wanaotembea chini ya majumba hayo kwa urefu wa mita 35.

Kampuni ya Eckersley O'Callaghan ambayo imeshirikiana na ile ya Apple kuhusu mtindo wa kidimbwi hicho cha kuogelea itatengeza mradi huo.
Kidimbwi hicho ni miongoni mwa miradi ya ujenzi ya maeneo ya kujivinjari kwa jina Embassy Gardens at Nine Elms,karibu na kituo cha umeme cha Battersea

Inatarajiwa kuwa mradi huo utakamilika ifikiapo mwaka 2019,lakini mtindo huo una changamoto zake hususan kutokana na hatua kwamba kidimbwi hicho kitazuiliwa na misukumo itakayotoka kutoka kuta za majumba hayo mawili ambayo yamejengwa na misingi tofauti.

''Upepo unapovuma majumba hayo huyumba tofauti na hivyobasi kuwa changamoto kwa watengezaji wa kidimbwi hicho'' kulingana na Brian Eckersley

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement