Kingwendu ambaye amekuwa akitumia maneno kama Eno! Eno huku! akitoa macho na ulimi nje, ameiambia Bongo5 kuwa yote hayo yatakuwa likizo.
“Unajua bungeni ni bungeni tu,” anasema. “Ile ni sehemu ya heshima, mbwembwe zangu zote nitaziacha, hata nikiwa nimepanick kusimamia hoja itanibidi niwe ngangali nisije nikachekesha watu,” ameongeza.
“Unajua nimekuwa mchekeshaji kwa muda mrefu sasa kuna vitu ambavyo vinaweza kuja bila kujizuia lakini nitajitaidi.”
Kingwendu anawania ubunge kwenye jimbo la Kisaware kwa tiketi ya CUF.
Chapisha Maoni