TAARIFA ZISIZO ZA KWELI ZA UWEPO WA MVUA KUBWA NA UPEPO MKALI KATIKA MAENEO YA DAR ES SALAAM, PWANI, TANGA, UNGUJA NA MTWARA
Mamlaka
ya Hali ya Hewa Tanzania inawatahadharisha wananchi kuhusu taarifa
inayosambazwa kwenye mitandao ya Kijamii inayohusu uwepo wa upepo mkali utakao
vuma kwa kasi ya km 123.7 kwa saa na mvua kubwa kwa siku ya tarehe 29/08/2015
kuanzia saa 7 mchana.
Taarifa
hii si ya kweli na kuwa Mamlaka ya Hali ya Hewa (TMA) haijatoa TAHADHARI hiyo.
Utabiri
sahihi wa kesho tarehe 29/08/2015 katika maeneo hayo ni kama ifuatavyo: Mvua
nyepesi zinatarajiwa katika baadhi ya maeneo hayo( Dar es Salaam,
Pwani,Morogoro, Tanga, Visiwa vya Unguja na Pemba).
Upepo
unatarajiwa kuvuma kwa kasi ya wastani wa kilometa 30 kwa saa katika
pwani ya kaskazini( Dar es Salaam, Pwani, Tanga pamoja na Visiwa vya
Unguja na Pemba) na kwa kasi ya kilometa 20 kwa saa katika pwani ya
kusini(Mtwara).
Aidha,
Mamlaka inapenda kuujulisha umma kuwa ina utaratibu maalumu wa kutoa tahadhari
kwa kutumia vyombo vya habari pamoja na mitandao ya kijamii
http://meteotz1950.blogspot.com/
na
tovuti yao ya
hivyo
basi Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania inatoa wito kwa umma kuacha kutoa na
kusambaza taarifa za kupotosha katika mitandao ya kijamii.
Imetolewa
na:
MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA
Chapisha Maoni