Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Kuku wakiwa wanauzwa sokoni

UKIPANDA daladala linalotoka Makumbusho kupitia Sinza ukifika kituo cha Shekilango, Makondakta wengi wamepabadili jina sasa panaitwa mahakama ya kuku.

Soko la Shekilango, Manispaa ya Kinondoni limejipatia umaarufu wa jina hilo kutokana na kuwapo kwa machinjio ya kuku.

Hata hivyo, Manispaa sasa imeamua kuifunga kwa muda usiojulikana kutokana na kukithiri kwa uchafu.

Machinjio hayo yalifungwa jana na Ofisa Mtendaji wa Kata ya Ubungo, Shabani Kambi baada ya kutembelea sokoni hapo ili kujionea hali ya usafi ilivyo.

Akizungumza mara baada ya kufunga machinjio hayo, Kambi alisema hadi sasa katika Kata yake kuna wagonjwa 11 wa kipindupindu ambao wanatoka mitaa ya NHC, Chuo Kikuu, Kibo na Msewe.

“Wiki iliyopita nilipita nikawaambia wazingatie usafi lakini leo (jana) nimekuja hapa naona hakuna kilichofanyika, sasa nafunga machinjio yote hadi mtakapojirekebisha,” alisema Kambi.

Licha ya kufunga machinjio hayo, Ofisa huyo pia aliwaamuru mama lishe wanaofanya shughuli zao katika maeneo mbalimbali ya kata hiyo kuacha biashara hiyo kuanzia leo hadi hali ya ugonjwa huo itakapotulia.

Katika hatua nyingine, Shirika lisilo la kiserikali linalojihusisha na masuala ya kijamii (CCI), limeanza kutembelea maeneo mbalimbali ya Manispaa ya Kinondoni ili kutoa elimu kwa wananchi kuhusiana na ugonjwa huo.

Ofisa Uhamasishaji masuala ya afya katika shirika hilo, Pudenciana Lukago, alisema elimu hiyo inatolewa kwa ushirikiano wa mtandao wa vikundi mbalimbali vya kijamii (Federation) vilivyoko kwenye Manispaa hiyo.

Aliyataja maeneo ambayo wamekwishatembelea kuwa ni Ubungo, Mburahati, Mwananyamala, Kigogo na Magomeni.

“Moja ya majukumu yetu ni kutoa elimu kwa jamii kuhusu usafi wa mazingira na kote ambako tumepita tumebaini watu wengi hawana elimu ya kutosha juu ya ugonjwa huu,” alisema Lukago.

Chanzo, MTANZANIA

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement