CHIPUKIZI anayekuja kwa kasi kwenye muziki wa kizazi
kipya, Amina Huseein ‘Mina’(Pichani), amesema anatamani kufanya kazi na mkali wa masauti,
Christian Bella.
Mina aliliambia gazeti la BINGWA kuwa, atakapofanya kazi na
Christian Bella ana imani ataweza kuongeza mashabiki wapya tofauti na alionao
sasa.
Christian Bella |
“Kufanya kazi na Bella naamini kiwango chake kitasaidia
kufika mbali ikiwa ni pamoja na kuongeza idadi ya mashabiki tofauti na hawa
nilionao ukizingatia sisi wasanii wa mikoani inakuwa ni ngumu kusikika,”
alisema Mina.
Chapisha Maoni