Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


 
MKURUGENZI Mkuu wa Ofisi ya Taifa ya Takwimu nchini (NBS), Dk. Albina Chuwa (pichani), amewashauri vijana kujitokeza kusomea fani hiyo ili waje kushika nafasi pindi walioko hivi sasa watakapostaafu.

Aidha amesema wakati umefika kwa watakwimu wa bara la Afrika kubadili mifumo ya uendeshaji kwenye ukusanyaji ili kuendana na hali halisi.

Rai hiyo ilitolewa mwishoni mwa wiki na Dk. Chuwa kwenye Maadhimisho ya Siku ya Takwimu Duniani, yaliyofanyika Dar es Salaam katika Chuo cha Takwimu Mashariki mwa Afrika.

Alisema hatua hiyo itasaidia kuziwezesha nchi za Afrika kufanikisha utekelezaji wa Malengo ya Maendeleo Endelevu (SDGs) yaliyopitishwa hivi karibuni na Umoja wa Mataifa (UN) kwa haraka.

“Kwa muda mrefu tumekuwa tukifanya kazi kwa mazoea, lakini wakati umefika kwa nchi zetu za Afrika kubadilika, ni lazima tushirikiane na wadau mbalimbali wa takwimu, hasa sekta binafsi, kwani wanazo takwimu nyingi hivyo tunahitaji kuzikusanya na kuziweka pamoja.

“Lazima tuwekeze kwa vijana kwa kuwafundisha kwa sababu itafika kipindi tunaweza tusiwepo, hivyo lazima vijana waingie kushika nafasi hizi ili wasaidie nchi zao na dunia kwa ujumla,” alisema Dk. Chuwa.

Alisema yanahitajika mabadiliko na kutumia njia za sayansi na teknolojia katika ukusanyaji wa takwimu ili kuendana na wakati tuliopo.

“Kazi ya kutumia njia za zamani katika ukusanyaji wa takwimu ni ghali, kwa mfano hapa nchini ili kufanya utafiti wa matumizi kwa kaya inagharimu kiasi cha Sh bilioni 12 pekee na hii si sensa ya jumla,” alisema Dk. Chuwa.

Dk. Chuwa alisema iwapo hatua hizo hazitachukuliwa kuna uwezekano siku zijazo mashirika makubwa duniani yatachukua nafasi za watakwimu wa mataifa mengine na hivyo hawa waliopo watapoteza nafasi zao.

“Ni vizuri sisi wenye nafasi hivi sasa tuwahamasishe wengine kujiendeleza kimasomo ili kujijenga kitaaluma na tuondokane na ule utegemezi wa kutumia wataalamu wa nje ya nchi,” alisema Dk. Chuwa.

Kwa upande wake, Makamu Mkuu wa Chuo hicho, Dk. Frank Mkumbo, alisema ili kupata takwimu zilizo bora ni lazima ukusanyaji wake uzingatie ubora katika uandaaji na usambazaji wa takwimu husika.

“Tunajitahidi kuyafundisha hayo hapa chuoni, tunazingatia suala la matumizi ya teknolojia, wanafunzi wetu wanatoka katika nchi zinazozungumza lugha ya Kiingereza, lakini kuna changamoto kwamba wengi hushindwa kusoma kutokana na kukosa ufadhili,” alisema Dk Mkumbo.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement