Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

Polisi akikagua uharibifu uliotokea baada ya ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata  ya Sandali ya Temeke Mikoroshini jijini Dar es Salaam kuchomwa moto baada ya wananchi kugomea matokeo

WANANCHI   wamevamia ofisi ya Mtendaji Kata ya Sandali Manispaa ya Temeke, Dar es Salaam na kuichoma moto wakitaka   matokeo ya udiwani wa kata hiyo yatangazwe.

Akizungumza na MTANZANIA jana, Mwenyekiti wa Mtaa wa Sandali, Deodat Chuma alisema kituo hicho kilichomwa moto saa 1:40  asubuhi, baada ya wananchi kukasirishwa na  kucheleweshwa  matokeo ikiwa pamoja na kutangazwa mshindi wa CCM, Abeli Tarimo.

Mwenyekiti huyo ambaye pia alikuwa wakala wa CCM, alisema  matokeo hayo baada ya kukatiliwa yalihesabiwa upya ambako wa CCM akaibuka tena kidedea kwa kuongoza kwa kura 600  wakati awali zilikuwa ni 400,  na mgombea wa CUF, Khalid Yahya aliyagomea.

“Matokeo ya awamu ya pili yaliongezeka tena kwa CCM kupata kura nyingi hali hiyo iliwakera   wenzetu wa upinzani,”alisema Chuma.

Alisema kutokana na hali hiyo kundi la vijana walivamia ofisi hizo ambako ndiko kulikuwa  ni kituo cha kupiga kura na kuichoma moto.

“Vijana hawa walidai wanataka kuchoma moto pia kituo cha afya, kanisa na shule ya msingi ikiyopo eneo hilo," alisema Chuma.

Chuma alisema amesikitishwa na kitendo hicho kwa sababu ni siasa chafu ambazo zimepitwa na wakati.

Alisema umefika wakati wanasiasa wakakubaliana na matokeo   wanapojitosa katika kinyang’anyiro mbalimbali.

Pia alisema katika tukio hilo nyaraka mbalimbali zimechomwa moto yakiwamo masanduku matatu ya kupigia kura ambayo yalikuwa matupu.

"Tunamshukuru Mungu matokeo yalikuwa tayari yamepelekwa kwa mkurugenzi hivyo hayakuchomwa,"alisema Chuma.
Akizungumzia vurugu hizo, alisema ilitokana pia na wakala mmoja kupoteza matokeo ya kituo cha Kisiwani ya udiwani ambayo hayajaonekana.

"Hii imetokana na Tume ya Uchaguzi (NEC) kutokuwa na mawakala makini… ndiyo yote haya yamesababisha,"alisema Chuma.

Khalid Komba ambaye ni wakala wa CUF, alisema uchaguzi huo haukuwa huru na haki na ulikuwa   wa mabavu.
Alisema tangu Jumapili Mgombea wa CUF, Khalid Yahya alishinda lakini hawakutaka kumtangaza.

Alisema  wamechoshwa na uongozi wa Tarimo wa CCM kwa kuwa ana miaka 15 ya uongozi ndani ya kata hiyo na hakuna alichokifanya.

"Huyu diwani anaishi Mbezi ikifika kipindi cha uchaguzi anakuja kuishi huku...hatumtaki kwanza hata CCM wenyewe wanafahamu alipita ‘kimagumashi’ katika kura za maoni ndani ya chama chao,"alisema Komba.
 
Wananchi wakishangilia nje ya kamba ya polisi baada ya ofisi ya Ofisa Mtendaji wa Kata  ya Sandali ya Temeke Mikoroshini jijini Dar es Salaam kuchomwa moto baada ya wanachi hao kugomea matokeo.
Alisema wao hawamtaki na wanachokifahamu hawana diwani kwa kuwa kura hawajampa yeye, aliyepewa hajatangazwa.
Mgombea   udiwani wa CUF, Yahya alisema fujo hizo zilitokea kwa sababu NEC haikutenda haki na kura nyingine walikimbia nazo.

Alisema polisi waliwatafuta mawakala wa NEC wakakamatwa watatu na hawakuwa na matokeo hayo waliwapa watu wa CCM ambao walikamatwa nayo.

Yahya alisema walitaka kubandika matokeo hayo bila kukubaliana kwa kuwa yalikuwa ni ya marudio na ni tofauti na ya awali.

"Wakati fujo hizo zinatokea mimi sikuwapo, wananchi wanamtaka mtu wanayempenda roho zimewauma na wana hasira,"alisema Yahya.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement