Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


UGONJWA wa malaria unaweza kuisha nchini iwapo serikali itasimamia kwa dhati sera na mikakati yake inayoipanga ikiwa ni pamoja na kudhibiti vitendo vya rushwa katika sekta ya afya.

kauli hiyo imetolewa jana jijini Dar es Salaam na Mkuu wa Kitengo cha Phatholog wa Chuo cha  Agakhan, Profesa Zul wakati wa uzinduzi wa dawa mpya ya kutibu malaria ijulikanayo kama Coartem 80/480.

“Takwimu zinaonesha malaria imepungua kwa asilimia 60 Tanzania lakini nchi ya Sirlanka imefanikiwa kuimaliza kabisa. Tatizo nililogundua ni kwamba kuna changamoto katika usimamizi wa utekelezaji wa sera na mikakati inayopangwa na serikali katika kumaliza tatizo.

“Hivyo ni vizuri serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Dk. John Magufuli ambayo inaongozwa na kauli mbiu yake ya Hapa kazi tu, kuzifanyia kazi changamoto hizo.

Alisema ingawa chanjo ya malaria ambayo bado ipo katika utafiti ina uwezo wa kuzuia malaria kwa asilimia 30 bado jitihada zinahitajika katika kupambana na ugonjwa huo.

Naye Msajili wa Baraza la Famasia nchini, Elizabeth Shekalaghe alisema kwamba ili kuendeleza mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria jamii inapaswa kuelimsishwa juu ya matumizi sahihi ya dawa.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement