Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement

 
ASILIMIA 80 ya watu wenye ulemavu wa ngozi hufariki dunia kila mwaka nchini kwa kukosa matibabu dhidi ya tatizo la saratani ya ngozi.
 
Akizungumza na MATUKIO NA MAISHA hivi karibuni jijini Dar es Salaam kuhusu Maadhimisho ya Siku ya Saratani duniani Ofisa Mahusiano wa Chama cha Albino Tanzania (TAS), Josephat Tona alisema hiyo ni kwa sababu huchelewa kufika katika vituo vya afya.

“Umri wa kuishi wa albino ni miaka 35 na 40 tofauti na watu wengine ambao hufika hadi kati ya miaka 50 hadi 70. Asilimia 80 wanafariki kwa sababu ya kuugua saratani ya ngozi ambayo kwa mujibu wa watalaamu inasababishwa na miale ya jua,” alisema.

Alisema ili kujikinga dhidi ya saratani hiyo huhitaji mafuta maalumu ya kupaka kwenye ngozi hata hivyo hushindwa kumudu gharama ya kuyanunua mafuta hayo.

“Naiomba serikali itenge bajeti itakayowezesha Albino kupata huduma za afya zilizo bora, itusaidie pia kupata mafuta ya kuzuia mionzi ya jua ambayo ni ghali na mara nyingi huwa yanatoka nchi za Ulaya, nakumbuka mara ya mwisho ilikuwa 2013 ambapo tulipatiwa jumla ya ‘tube’ 4000 za mafuta za kugawa nchi nzima ambayo kimsingi hazitoshi,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement