Akina mama wenye watoto wachanga
nchini Kenya wataweza kwenda kazini na wanao. Hii ni baada ya bunge
kupitisha mswada wa Afya ambao utalazimu kampuni kutenga maeneo maalum
ya kuwanyonyeshea watoto.
Chini ya mswada huu waajiri lazima watoe muda kwa wanawake kuwanyonyesha watoto hao, kwa kupokezana.
Rachel Nyamai, mbunge aliyewasilisha mswada huo amesema utasaidia wanawake kufanya kazi vyema na wakati huohuo kuimarisha afya ya mtoto.
Chumba maalumu cha watoto |
Hii imewalazimu wanawake wengi kuwacha kuwanyonyesha watoto wao mapema kutokana na masharti na majira ya kazi.
Pendekezo sawa na hili lilitupwa nje na bunge lililopita baada ya tume ya waajiri kulalamika na kutishia kuwanyima kazi wanawake.
Mswada wa sasa wa Afya 2015 utawasilishwa kwa bunge ili kuidhinishwa kuwa sheria.
Chapisha Maoni