Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


WAJASIRIAMALI zaidi ya 50 Visiwani Zanzibar  wamepatiwa mafunzo maalumu na benki ya Afrika Tanzania ili kuwajengea uwezo wa kibiashara na kiuchumi.

Mafunzo hayo yalitolewa mwishoni mwa wiki visiwani humo na ikiwa sehemu ya uzinduzi wa Benki ya Afrika Tanzania tawi la Zanzibar  katika  Kuhakikisha utekelezaji wa mpango wa ukuzaji wa mtandao wake nchini.

Mwenyekiti wa Bodi ya wakurugenzi wa benki hiyo, Balozi Mwanaidi Sinare Maajar katika uzinduzi huo alisema  imewekeza katika kustawisha uchumi wa Tanzania kwa  kueneza matawi yake kwenye maeneo mbalimbali ya Tanzania katika mikoa ya Arusha, Dar es Salaam, Dodoma, Kilimanjaro, Mwanza, Mbeya,  Morogoro, Shinyanga,  na Mtwara.

Mwanaidi aliongeza kuwa tawi hilo lililozindiliwa Visiwani humo ni la 22 kwa Tanzania ambapo mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka 2015, BOA ilifikisha faida ya bilioni 7 za kitanzania kutokana huduma bora zinazoendelea kutolewa sehemu mbalimbali nchini.

Alisema kuwa wamechagua Zanzibar kutokana na uwezo wake mkubwa Hasa katika kilimo cha viungo, uvuvi, biashara na utalii,ambapo huduma za kukidhi mahitaji kwa wananchi zitatolewa kwa ubora unaotakiwa.

 Naye waziri wa fedha wa serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar Omar Yussuf Mzee, aliyekuwa mgeni rasmi katika ufunguzi huo alisema kuwa Serikali inatambua kwamba maendeleo ya kukuza uchumi na kuondoa umaskini hayawezi kufanikiwa bila ya kushilikisha Sekta binafsi pamoja na sekta ya kibenki.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement