Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement



 
RAIS wa Rwanda, Paul Kagame anatarajiwa kuwa mgeni rasmi kwenye kongamano la biashara, viwanda na usafirishaji linalotarajiwa kufanyika Mei 20 mwaka huu Kigali Rwanda.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Makamu mwenyekiti wa Chama Cha Wafanyabiashara, Viwanda na Kilimo Tanzania, Dk Kingu Mtemi alisema kuwa, lengo la kongamano hilo ni kutoa fursa za kibiashara katika sekta mbalimbali ikiwamo, viwnada, nishati na madini, usafirishaji na kilimo.

Alisema kutokana na hali hiyo, zaidi ya wafanyabiashara 100 kutoka Tanzania wanatarajiwa kushiriki kwenye kongamano hilo hali ambayo itaweza kuleta ushirikiano wa karibu na kuongeza uzoefu.

“Tunatarajia kupeleka wafanyabiashara zaidi ya 100 kwenye kongamano hilo ili waweze kupata fursa ya kubadilishana mawazo na kuongeza masoko katika shughuli zao,”alisema Mtemi.

Aliongeza, hali hiyo itasaidia kukuza uchumi na kuongeza mapato jambo ambalo linaweza kusaidia kuongezeka kwa ushirikiano wa karibu baina ya nchi hizo mbili.

Alisema, mpaka sasa, zaidi ya asilimia 80 ya bidhaa zinazokwenda nchini Rwanda zinatumia bandari na magari ya Tanzania, jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa, nchi hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kukuza uchumi.

“Kila mwaka tunapata bidhaa zaidi ya asilimia 800 ambazo zinatoka nchi mbalimbali kwenda Rwanda kupitia bandari ya Tanzania, lakini pia bidhaa hizo zinasafirishwa na magari yanayotoka kwenye kampuni za hapa nchini, jambo ambalo linaonyesha wazi kuwa, nchi hiyo inachangia kukuza uchumi,”alisema.

Alisema, kutokana na hali hiyo, wafanyabiashara hao wataparta fursa mbalimbali ambazo zitawaongezea kipato na kuleta mahusiano wa karibu kwa wahusika.

Alisema, mkakati uliopo ni kuhakikisha kuwa, wadau wa kongamano hilo wanatoa elimu  kwa wananchi na wafanyabiashara kwa ujumla ili waweze kujitokeza na kushiriki kwenye kongamano hilo kwa ajili ya kuongeza uzoefu.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement