Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?view=att&th=15451fb662a87875&attid=0.5&disp=inline&realattid=1532666061499924480-local4&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-OWemFJp03jzCM_uhOVf7a4NQum5Q9j4S6yuXUXT3PLzIV_ny9JsHvl2KmsVTlL3jl8SEth6gsN8fLDwJUjAcolRNb5ot7z7vTkJekwSvRVmb1hjSot31PgFNRXFTmU1a8LwOWF3sEuKZr4coL0Hj2X8Ye9cId4Z76WlMa1Dw23bDQJwcFh-zR8XM87nQ2JhpVn_Td7iji4_etb9Rd7SlhvK-cfk5PvucTPHOkQIZcUpirCo8_aNgMBDmA-ZdcOpWYmKvD0rjeYWzmrWOgsV0UM5x1SkkX3mM6dyHXVUxrcJmRPsNIr9Zf5y2NWP0qljtS-mLPxYFYH57adQYprVnyvWXHV7VOxdfBBLzqXkEWAEh1AaG-Z1R8tDfcevOILufKtI5klQqeg4zRre8nufbpF2VaQ2eKRmJ5NWdsOQCuyp1Clgpb9bNorJXSnzAKh4hW961dYRBV_k6h97X768RWrChkv_TjQri0X8A6mjWwsu0o3riY_5Gw4V5xsxXtQaannUPGX86S7fpXdwPT0vAgE4_ScoKALhLhdmjy23DXJsOPlm-X_DDoR4SIvA-CQZocFMWU3KeXWoSr0LwHLnXx7yOBhPEMXaODCt2J47O1i46KDfQd4ZNKDDKUUs4ScTw6ZX230bM_qzqK 
Tanzania jana iliungana na mataifa mengine kuadhimisha siku ya malaria duniani. Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Ummy Mwalimu aliadhimisha kwa kuwaongoza waandishi wa habari huko mjini Dodoma kupima malaria kwa kutumia kipimo cha haraka (mRDT).

Baada ya shughuli hiyo Waziri Ummy alitoa tamko rasmi ambapo alisema ugonjwa huo bado ni tishio hasa kwa maeneo ya vijijini kuliko mijini licha ya takwimu kuonesha umepungua hadi asilimia 50 toka mwaka 2007/8 hadi 2011/12.

Kiwango cha maambukizi katika maeneo ya vijijini ni asilimia 10.7 na mijini asilimia 3.4.

'Kupungua kwa kiwango cha maambukizi ya malaria kunatupa sababu ya kujipongeza na kumshukuru kila mdau aliyechangia kwa namna moja au nyingi katika jitihada hizi lakini bado tunatakiwa kupambana na kufikia lengo letu la kupunguza kiwango hicho hadi kufikia asilimia 5," alisema
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?view=att&th=15451fb662a87875&attid=0.4&disp=inline&realattid=1532666061499924480-local3&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ9wrLR7QcC7IzlWD4FcqNUOY6Ae1saWPFjfx8aYw4t_YzwhACH4nDNknTgVqfP2z_PkWJCleaeFErVgVhhKdGzz-yHpVimKXXCcrgQj4bqwSiVFGBZwu7uXhzT-YY1rfCygos2ZoxaRBL-oMNj4Dl5aSCEsa1PIR7BH05tkTQoAgl5b0VdSbEmAqDd5eNIsYLgOIgFwZ_3hA6uBmv94UyVUthsRrfXMDjssxA9S5c2fDfd40JY5A64NwFaK9QNp-VvqKnCCQYc0lZAXGxIeMtPaq_WMCpGoo6Qtaq0hqpKvk1jIjSN5bkW45JkTLzJejsfHAUMPbD6SttZitOWV9KxIobm0WNt47tPK5FkIcM_Ad-MMoS2ItqqjCjfm6xvPmP3aQcVeNvSIWJzFWgP9VMrgYb5tBed9DwtkAcfX3MlMo_K48Eavbs5sU6vpj4JTpVg1Kqa7aFUPcAIygGc0MhfUnCN4rjgey7F5HDjD6HjZqL7-FFNgykQS3iH6gIiLuPy5Q9_oZI_mrtTO7s6_3EGTtC7GyPKnaB6Ly35jvk9PYEupRvOabAspbRllMaor6_bmAHAthNSyP2ClnPiyyqlMtjJj6EK1rxO4-mC88SOiqhFrxKsq6Xahqh41jtNf_V6bIHdidtlLF4oU
Takwimu za vituo vya afya zinaonesha kuwa takribani watu milioni 12 hupata ugonjwa wa malaria kila mwaka hapa nchini huku makundi yanayoathirika zaidi ni watoto wenye umri chini ya miaka mitano (5) na mama wajawazito.


“Ikumbukwe ugonjwa huu wa malaria  ni hatari kwa uhai wetu, maendeleo na ustawi wa Taifa letu, na ndiyo moja ya sababu kubwa inayochangia katika kupunguza kasi ya maendeleo  ya jamii, hii ikiwa ni pamoja na kuleta vifo na madhara mengine yatokanayo na malaria” iliongeza taarifa hiyo.
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?view=att&th=15451fb662a87875&attid=0.3&disp=inline&realattid=1532666061499924480-local2&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-TZZ4Hp2nSEEVb1ktyrRz_qjhJ773rlV-6tKWwYFNhOll12jSpOqlmGa0amzcrUAoxH0Qq-aDPMAMvXF0yuLHva9DNFt3uxnGw8FwC6fpyFwv7aE3_s53oN5KYcuQr9weuW5h4PBVe6b409CjMgp9Z-cSOky-L5aaxHX8N33ZAaT-8TBcbX0Dnfen3czear2RWLDXlHJAYHUzKghoM9DGuJ9QQoxTfGi9qpSCXOsnEs24sQ1aFMzGm-e06g78ElQmpUGJt3-TzhgWj16q5rwrOzsWm7ji1VBwAir0vIthWE_R5vHboDP9CYHlYaPspdrmsf0sauclFfW-duiuwyX5mJxTSqdI70Iem-ohkMLy_hSzRJQuKfAEOpsHGDNWWhVLxwhPs0T_uxhrJfoAkTZmWkgbV4FqB_9NojJgyrdccnkL1zAA22pYEMy45fSQOUGs1Y6oH_SOmg_pLn95Tt0lvJz3w_PTBmKUXe4zRMDYbm9lM3t8XeCyLzvH60EABgu0w1fZthV7hXnqeQOorkr_0seGmoQ0jCvfeVem0Hvwagdt3U1TOfjJs-3BUPUhDKq3JLo190vLFSWj_LGmWI-FnYjawojdDR-YVbn2oMO5CoHhVjlo1JQvLNTDGwZVRyHKKDbQdCeyHFD3V
Waziri aliwataka wananchi na wadau wote kuona umuhimu na kushiriki katika mapambano dhidi ya ugonjwa wa malaria kwa kuhakikisha matumizi sahihi ya mikakati ya kuuthibiti ugonjwa huo, na kusema kuwa iwapo mikakati hiyo itatekelezwa ipasavyo ni dhahiri kuwa maambukizi yataendelea kupungua kwa kiasi kikubwa na hatimaye kumaliza kabisa tatizo hilo.
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?view=att&th=15451fb662a87875&attid=0.1&disp=inline&realattid=1532666061499924480-local0&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ9i18ix78CHqE-Mman9dHnYrBkevmBaQHZGeIIkobMZIVpDJdFsJfN_8O3fzwdDwAmQsjBHlCrAokBlOgipGhtiqby1kYleIP2OuTzggnI-e2j5zaJzQDzNLwzGKVlclrQriS7Z_gfHlehMQNMTcu4209zu9GuDJTYICDWgX0ixTqm2m8C8sXEDu5nbs7Zhr93hzEWJEBSjL8Q7dwbD9m8qzrnINwuHOo9tp1EB_qZwwrV3IEZcqsHHuUOlWPJsTzLKYXxtD_47AKtzgJHCRf0S1VHqIvhf_N1yFZSuUSwO_EShjL5TqUcRCdPnoDjD7E1Obdp8bUOYqlAG-g4yqu265fjlvoBMVDoCBJZUi1SlGjUEwa9DNgPBWFYGUxuVO0EfIQfS5afE4mvQ7tooyFeeOnvibszEG5f4Bpxawqng_5P-E-K2uBdKbSklcFLiCoPkCGFb8Em3Fkp_3D7jFBXeybcrLwTLXxQSyTMRSYy5HR1wtQjSK54pQn8mHmbj8vK4nwkZZEmHKuvt_fj-W0AHn-ENQimvQgRzIrtow0sd_ZTP7AqA-m3ICCcXljGyeUMH9mk8I2Cw509ZUTqHRRTwUOqGd2bW40sbhMwc42ivo-7BAR76SbLmUDgDpUvQZ8SD4E4-C_MuAiyj
Alisema mikakati inayotekelezwa na Wizara  kwa kushirikiana na  wadau ni pamoja na Udhibiti wa mbu kwa kutumia njia mbalimbali, kama vile kutumia vyandarua vyenye viuatilifu vya muda mrefu; unyunyuziaji wa viuatilifu ukoko katika kuta ndani ya nyumba, kusafisha mazingira na kuua viluwiluwi vya mbu kwa kutumia viuadudu vya kibailojia hasa katika maeneo ya mijini.
https://mail-attachment.googleusercontent.com/attachment/?view=att&th=15451fb662a87875&attid=0.2&disp=inline&realattid=1532666061499924480-local1&safe=1&zw&saddbat=ANGjdJ-VGeWHCYrvEh3aDQZWiKetMK5ap1ojpmqZkiM40OgILO4LPIzkUZwK6LQvrQw5967pIBWUGrahBMLnh968FGxDyObcVuOO1LxALVvFM70zN01l2TjFw-8w2Zs4xkVDJeF4XJ2I-QugFZMrNQ7BPP6KuKB0khHE9E304dmyLbSFFtDv4LYlfmh8G4o_gh1Jzr-mxpIB4v03vmjttZd--l4ePOsSQu5PqDXhb9g-FOumtZeg2OcoZbFoVLktRsbEQ2Mes_VhhtZ41GodvYZtGSW2cqIACPctAalRiQVJw36KPGG6XkAbfgfby7PtUThN0bAyppm7bEegoEuLvatlnff057fhjiPPVUrI9-pnUyt4Y8NGzq7Ez-UCEb9eAZbldlkTBpYKEBFQXgWfLXtV3cwhWpWchtsNVMboZBTM87XT2_DZzXdKNuqcXsY-EOZO0WBf_1B0BUI1uNml2ZmXtOnqVf9-y3zN83dVGxjKowiD8-g4dgbXFrWpC-wVknQe_WRo21vbzQBbxZqJix7fieweW7LR7rx9mRTktEgl68TKcxGpZFIHJJ4gMCJInQKl5MV-TDGT_qnMr6O3Fqyrfj_5evDjSYquRAv6bqZVotD1MNxq-G7Wg1AjxVyCFw2MLkUHXKQ65076Cbsq
Waziri Ummy alisisitiza wananchi kuzingatia kupima ili kujua uwepo wa vimelea vya malaria kabla ya kutumia dawa, kumaliza kozi ya dawa kulingana na maelekezo ya mtoa huduma, kutumia vyandarua vyenye viuatilifu kila siku wakati wa kulala, kuzingatia usafi wa mazingira kuzuia mazalia ya mbu.



Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement