Recent Post


 


moja

Responsive Advertisement


 
WASANII mahiri wa muziki wa bongo flavor akiwamo Vanessa Mdee, Navy Kenzo, Weusi, pamoja na kundi la vichekesho la ‘Orginal Comed’ wamekubali kujitolea kuelimisha jamii juu ya ugonjwa wa sickle cell.

Kauli hiyo ilitolewa jana jijini Dar es Salaam na  Mwanaharakati wa masuala ya sickle cell, Uingereza Yasimin Razak alipozungumza na waandishi wa habari.
 
“Kwa mujibu wa takwimu za Shirika la Afya Duniani (WHO) Tanzania inashika nafasi ya nne kwa kuwa na idadi kubwa ya wagonjwa wa sickle cell, na wataalamu wanasema ni tatizo linalowapata watu weusi pekee,” alisema 

Alisema hata hivyo jamii haina uwelewa wa kutosha juu ya ugonjwa huo hivyo amejitolea kushirikiana na wasanii kupeleka elimu.

“Nilikutana na wasanii wengi mwishoni mwa wiki na hawa ni miongoni mwa wasanii walioonesha nia ya kushiriki katika kampeni ya kuelimisha jamii ambayo natarajia kuifanya Juni 19, mwaka huu ambayo ni siku ya Sickle cell duniani,” alisema.

Post a Comment

saba

nane


 


sita

Responsive Advertisement