Meneja Mauzo na Usambazaji wa Kampuni hiyo, Fred Kazindogo |
Kampuni ya Dar Brew ambao ni wazalishaji wakuu wa bia ya
asili ya Chibuku imesema bia hiyo maarufu kwa jina la Chibuku super itaanza
kuuzwa hadi kwenye maduka makubwa (Super Market) nchi nzima kwa bei ya Sh. 1000.
Meneja Mauzo na Usambazaji wa Kampuni hiyo, Fred Kazindogo
alisema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa uzinduzi wa chupa yenye
muonekano mpya wa Chibuku super yenye ujazo wa milimita 750.
“Chibuku Super itaanza kupatikana nchi nzima katika baa,
maduka makubwa ‘super market’ katika maduka ya jumla na rejareja na sehemu
zinazouzwa vileo kuanzia leo. Nina imani kubwa wapenzi wa bia yetu wataipokea
kwa shangwe na wataitumia ili kuonyesha kuwa wanajali asili yao,” alisema Kazindogo.
Naye Meneja Masoko wa Kampuni hiyo, Oscar Shelukindo (mwenye miwani) alisema
mtumiaji atakayenunua kinywaji hicho hatalazimika tena kurudisha chupa mahala
aliponunua na kwamba imewekwa katika chupa nzuri ya plastic inayovutia.
“Bia hii imetengenezwa kwa utaalam wa hali ya juu na kwa kutumia
mitambo ya kisasa kabisa, hivyo tunawahakikishia watumiaji ubora wa hali ya juu,”
alisema.
Chapisha Maoni